Yanga Yaiua Simba Yatinga Fainali Tusker Cup

Friday, December 25, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


YANGA imefanikiwa kutinga fainali ya Kombe la Tusker baada ya kuifunga Simba mabao 2-1 kufuatia mchezo wa nusu fainali uliochezwa leo jioni kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Yanga ndio waliokianza kipindi cha kwanza kwa kasi na kusukuma mashambulizi langoni mwa Simba katika dakika ya kwanza tu ya mchezo nusura waandike bao baada ya mabeki wa Simba na kipa wao Juma Kaseja kujichanganya lakini Jerry Tegete akawa mziko kuuwahi mpira uliokuwa unazubaa.

Wanajangwani waliendelea kushambulia mfululizo lakini katika dakika ya tano, Simba walizinduka na Mussa Hassa Mgosi alipiga shuti kali lililokua linajaa wavuni lakini kipa Mghana wa Yanga, Yaw Berko aliliona na kupangua na kuwa kona tasa.

Dakika moja baadaye, Mrisho Ngassa aliambaa na mpira tokea katikati ya uwanja huku mabeki wa Simba wakishindwa kumthibiti na alifanikiwa kupiga krosi ‘ndizi’ ambayo hata hivyo beki Kelvin Yondani aliiwahi na kuitoa nje na kusababisha kona ambayo hata hivyo haikuzaa bao.

Kiungo mpya wa Simba, Jerry Santo nusura aipatie timu yake bao katika baada ya kuachia shuti kali pembeni mwa uwanja lakini mara nyingine, Berko alikuwa makini na kupangua mpira huo uliozaa kona.

Kwa ujumla katika kipindi cha kwanza, Yanga ndio waliotawala kipindi cha kwanza na kufanya mashambulizo mengi zaidi wakifanikiwa kutengeneza nafasi saba za kkufunga huku watani wao Simba wakitengeneza nafasi tatu tu.

Katika kipindi hicho Yanga ilipata kona tatu na watani wao Simba wakapata tatu lakini hakuna iliyozaa bao. Huku mwamuzi kutoka Uganda akiwazawadia kadi za njano wachezaji Amir Maftah, Ngassa (Yanga), Yondani na Emmauel Okwi (Simba).

Yanga ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 67 kupitia kwa Jerry Tegete baada ya pasi nzuri iliyopigwa na Abdi Kassim kuuvuka ukuta wa Simba uliokuwa ukijichanganya tangu mwanzo wa mechi.

Baada ya bao hilo Simba walionekana kuchanaganyikiwa na kuwapa nafasi Yanga kushambulia zaidi hata hivyo hawakuwa makini kumalizia.

Dakika ya 78 Okwi aliangusha ndani ya eneo ya eneo la hatari na Cannavaro na mwamuzi kuamuru penalti ipigwe na Hilary Echesa akafunga kwa ufundi huku kipa Obren Cuckovic aliyeingia katika kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Berko aliyeumia akishindwa kuzuia.

Mabao hayo yalidumu hadi dakika 90 na mwamuzi Dennis Batte wa Uganda kuamua kuongeza dakika ambapo katika dakika ya 120, Shamte Ally aliipatia Yanga bao la pili na laushindi baada ya kuitumia vema pasi ya Mrisho Ngassa.

Kwa matokeo hayo, Yanga itacheza na Sofapaka katika mchezo wa fainali keshokutwa Jumapili.

source.nifahamishe

Adakwa Live Akiwabaka Farasi

Friday, December 25, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja wa nchini Marekani ambaye alikodisha nyumba karibu na uwanja wa mashindano ya farasi ili aweze kupata nafasi ya kufanya mapenzi na farasi, amedakwa live akiwa juu ya farasi.
Kijana Erick Rivera mwenye umri wa miaka 18 anakabiliwa na mashtaka matano ya kuwafanyia ukatili wanyama baada ya kunaswa akifanya mapenzi na farasi.

Taarifa zilizotolewa na polisi zilisema kwamba Rivera alikodisha chumba karibu na uwanja wa mashindano ya farasi wa Hudson Valley uliopo Goshen, Indiana ili aweze kumalizia haja zake za kimapenzi kwa farasi waliokuwa wakihifadhiwa kwenye mazizi ya farasi yaliyopo kwenye uwanja huo.

Kuanzia mwezi julai mwaka huu uchunguzi wa polisi ulianza katika mazizi ya farasi hao baada ya watu wanaowatunza farasi hao kukuta stuli kwenye mazizi hayo.

Baada ya uchunguzi wa polisi wa miezi sita iligundulika kuwa Riviera alikuwa akiwanyatia farasi hao nyakati za usiku na kufanya nao mapenzi.

Polisi walifanikiwa kupata video za kamera za ulinzi zikimwonyesha Rivera akifanya kitendo hicho.

Rivera amefunguliwa makosa matano ya ukatili kwa wanyama na kufanya wizi.

Rivera ametupwa mahabusu akisubiri hukumu yake huku dhamana yake ikiwa ni dola 15,000.

source.nifahamishe

Faza Krismasi Safari Hii Hakutoa Zawadi, Apora Pesa

Friday, December 25, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Faza Krismasi huyu wa nchini Marekani hakuwa kama wenzake, hakuja kwa nia ya kutoa zawadi kama kawaida, yeye alivamia benki na kupora pesa.
Mwanaume mmoja wa nchini Marekani akiwa amevalia mavazi ya Faza Krismasi (Santa) aliiteka benki katika mji wa Nashville, Tennessee na kupora pesa na kisha kutoroka.

Faza Krismasi huyu ambaye tofauti na wenzake ambao hubeba zawadi, yeye alibeba bunduki na kuwatishia wahudumu wa benki ya SunTrust Bank wasalimishe pesa zote walizo nazo.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na polisi, faza krimasi huyu wa bandia jana asubuhi aliingia kwenye benki hiyo akiwa na kiroba chekundu ambacho alikiweka juu ya meza ya mhudumu wa benki na kisha kutoa bunduki yake akiwaamuru watu wote waliokuwepo kwenye benki hiyo walale chini.

Baada ya kukijaza kiroba chake pesa, faza krismasi huyo alitoka taratibu na kupanda gari la rangi ya kijivu lililokuwa likimsubiria nje ya benki hiyo.

Wakati akiondoka zake, faza krimasi huyo aliwaambia watu waliokuwepo kwenye benki hiyo kuwa "Faza Krismasi anahitaji pesa za kuwalipa wasaidizi wake".

Kiasi cha pesa kilichoibwa toka katika benki hiyo hakijajulikana na polisi wameanzisha msako wa kumtafuta faza krimasi huyo feki.

source.nifahamishe.com

BREAKING NEWS - Mwanamke Ampiga Mwereka Papa Benedict Wakati wa Misa ya Krismasi

Friday, December 25, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamke mmoja wa nchini Italia anashikiliwa na polisi baada ya kuruka vizuizi vya ulinzi na kumpiga mwereka Papa Benedict XVI wakati akielekea kufungua misa ya krismasi katika kanisa la St. Peter mjini Vatican.
Mwanamke aliyefanikiwa kuruka vizuizi vya ulinzi, alimpiga mwereka Papa Benedict XVI aliyekuwa akielekea mbele ya kanisa kuanzisha misa ya krismasi katika kanisa la St Peter mjini Vatican.

Katika tukio hilo lililotokea usiku wa kuamkia leo ijumaa, Mchungaji Ciro Benedettini aliyekuwa karibu na Papa alisema kuwa Papa aliamka kutoka chini mwenyewe baada ya kuangushwa na mwanamke huyo.

Papa mwenye umri wa miaka 82 hakupata jeraha lolote katika tukio hilo lakini alionekana kutetereka wakati walinzi na wasaidizi wake walipokuwa wakimuongoza kuelekea kwenye altare kuu kuiongoza misa ya krismasi.

Mchungaji Benedettini alisema kuwa mwanamke aliyemwangusha chini Papa alionekana kuwa na matatizo ya akili na alikamatwa na polisi wa Vatican.

Pia mwanamke huyo alimsukuma na kumwangusha chini kardinali Roger Etchegaray, ambaye alipelekwa hospitali kwa uchunguzi zaidi wa afya yake.

Baada ya tukio hilo Papa aliiongoza misa ya krismasi kama kawaida na hakugusia hata kidogo tukio la kuangushwa chini na mwanamke huyo.

Aliianzisha misa ya Krismasi kama ilivyo desturi kwa maneno ya kilatino ya kuwatakia watu amani kwa kusema "Pax vobis" ("Amani iwe juu yenu") na waumini walijibu "Et cum spiritu tuo" ("Iwe juu yako pia").

Hii ni mara ya pili kwa mwanamke kuruka viunzi vya ulinzi na kujaribu kumdondosha Papa. Wakati wa misa ya mwaka jana, mwanamke mmoja aliviruka vizuizi vya ulinzi na kumfikia Papa lakini kabla hajafanya chochote walinzi walimwahi na kumweka chini ya ulinzi.

Haijajulikana mara moja kama mwanamke aliyemdondosha Papa safari hii ndio yule yule wa mwaka jana au la.


source.nifahamishe

mtanzania aliyeuawa uingereza

Wednesday, December 23, 2009 / Posted by ishak / comments (0)



Salum Kombo,mtanzania alieuawa nchini uingereza
href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjxW6wnbAqtiI4fB_Bt15m4-dUUfKSrPfStobmzK5E30sEM0zcGyFsjgbHhC82iZtNGOqX3S5rpOruqb_JOFLgsn6EMU-U_ObzA2Gh4ry29dY1kiKPSqwaYqqdrgh6BgkjFQSBs-QvP6jEB/s1600-h/1261554632_marafiki_wa_kombo.jpg">
marafiki zake wakimlilia kwa huzuni kubwa

sehemu ya tukio lilipotokea
SALUM KOMBO, kijana mwenye umri wa miaka 18, Mtanzania ambaye ameishi Uingereza kwa muda wa miaka ipatayo saba, jana ameshambuliwa kwa kisu na kufa kutokana na kilichoelezwa kuwa "mgogoro mdogo" uliotokana na mtandao (tovuti) unaotumiwa na watu, hususani marafiki au watu wenye uhusiano wa karibu, kuwasiliana juu ya mambo mbalimbali uitwao Facebook...

Uzio wa Hoteli ya kitalii wabomolewa ni siku tatu toka izinduliwe na R

Wednesday, December 23, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


UZIO WA HOTELI ya kitalii iitwayo Snow Crest ya jijini Arusha, imebomolewa uzio uliozunguka hoteli hiyo na kuharibu miundombinu mizima ya mawasiliano hotelini hapo baada ya kudaiwa kuwa umejengwa kwenye eneo la hifadhi.
Ukuta huo ulibomolewa jana majira ya saa 11:30 za asubuhi, na Wakala wa barabara nchini [TANROADS] kwa kudai uzio huo umejengwa kimakosa na umezidi eneo la hifadhi ya taifa.

Hatua hiyo ya Tanroads imekuja ni baada ya siku tatu toka Rais wa nchi, Jakaya Kikwete kwenda kuzindua hoteli hiyo ya kitalii mjini humo Ijumaa wa wiki iliyopita.

Meneja wa Hoteli hiyo Bw. Mark Digira aliwaambia vyombo vya habari kuwa Kutokana na kuvunjwa kwa ukuta huo imeharibu hadhi ya hoteli hiyo ambayo I imejengwa kwa mabilioni ya fedha.

Na kusema kuwa labda kuna hujuma maana kama kungekuwa na kasoro hizo wakala wa barabara wangezuia toka hoteli hiyo inajengwa lakini amewsema wao hawakupata kibali chochote kutoka kwenye taasisi hiuyo iliyoashiria wasijenge eneo hilo na ingekuwa hivyo wasingeweza kufanyia hivyo.

Amesema hoteli hiyo iligharamia kiasi cha shilingi bilioni 8 za kitanzania kujenga hoteli hiyo ya kitalii iliyozinduliwa na Rais Kikwete.

Wakizungumza na vyombo vya habari ene o la tukio, wakala hao wa barabara walisema sababu iliyofanya ibomoe uzio huo ni Kutokana kujengwa na kuchota mita 22 na nusu ya hifadhi ya taifa.

Wamesema hiyo ndiyo sababu kubwa iliyofanya uzio huo ubomolewe kwa kuwa walimega eno hilo ambalo haliwahusu kwen yeujenzi huo wa hoteli.
Hoteli hiyo ya Snow Crest ipo mijini Arusha kwenye barabara iendayo Moshi Arusha.

HAta hivyo wadau mbalimbali wakiwemo na wakazi wa mjini humo kitendo cha Tanroads kimechukuliwa ni sawa na kumdharau rais Kikwete aliyekwenda kuzindua hoteli hiyo.

source.nifahamishe.com

Mtoto Yatima wa Miaka 10 Amuua Mama Aliyejitolea Kumlea

Wednesday, December 23, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Mtoto mwenye umri wa miaka 10 wa nchini Thailand ambaye alinusurika kufariki wakati wa tufani la Tsunami nchini humo lililowaua wazazi wake wote wawili, amefunguliwa mashtaka ya mauaji ya mwanamke aliyejitolea kumlea ambaye alikuwa akimbeza kuhusiana
Polisi wa Jakarta Indonesia walimfungulia mashtaka mtoto huyo baada ya kumkuta mwanamke aliyejitolea kumlea Etty Rochyati mwenye umri wa miaka 55, akiwa amefariki baada ya kupigwa na kitu kizito na kuchomwa chomwa na kisu tumboni, limeripoti gazeti la Jakarta Globe .

Maiti ya mwanamke huyo ilikutwa kwenye kiambaza cha nyumba yake akiwa na majeraha mengi kichwani na majeraha ya kisu tumboni mwake.

Mtoto huyo ambaye jina lake halikutajwa kwa sababu ya umri wake mdogo, aliwaambia polisi kuwa mwanamke huyo alikuwa akimnyanyasa kwa maneno akimwambia “Hujui kuwa wewe huna baba wala mama?” na wakati mwingine alikuwa akitishia kumfukuza nyumbani kwake asipofuata amri zake.

Mtoto huyo alinusurika kwenye gharika la Tsunami lililokiteketeza kijiji chake kwenye kisiwa cha Nias ambapo wazazi wake wote wawili walifariki.

Mtoto huyo anakabiliwa na kifungo cha miaka 15 jela iwapo atapatikana na hatia lakini taasisi ya kutetea haki za watoto nchini humo inapigania mahakama imhukumu mtoto huyo kama mtoto na hivyo kutoa adhabu ndogo.

“Kitu alichokifanya mtoto huyu kinaweza kuhesabika kama kitendo cha kujilinda kutokana na manyanyaso na wala hakukusudia kufanya kitendo hiki”, alisema katibu wa taasisi hiyo Arist Merderka Sirait.

“Hapa hatudili na kesi ya mwanaume wa miaka 22, tuna mtoto wa miaka 10 ambaye hajui chochote na ambaye ana maisha marefu baadae”, aliongeza katibu huyo.

Katibu huyo alisema kuwa familia ya mwanamke aliyeuliwa imekubaliana kuifuta kesi dhidi ya mtoto huyo na wapo katika taratibu za kuwasiliana na maafisa wa upelelezi na wanasheria kujua mustakbali wa kesi hiyo.


source.nifahamishe.com

Mfanyabiashara wa Kihindi Akamatwa na Kilo 8 za Almasi

Wednesday, December 23, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Mfanyabiashara mmoja toka India amekamatwa nchini Jamhuri ya Kongo akiwa na begi lililojaa zaidi ya kilo nane za madini ya almasi yasiyosafishwa akijaribu kuyasafirisha madini hayo kinyemela toka nchini humo.
Mfanyabiashara huyo aliyetajwa kwa jina la Ajudiya Pravin Kumar amehukumiwa kwenda jela miezi sita pamoja na kulipa faini ya dola laki moja za Kimarekani.

Kumar ambaye ni mfanyabiashara wa madini ya almasi alikuwa akiendesha biashara zake nchini humo kwa zaidi ya miaka sita.

Kumar alikuwa akitafutwa na mahakama kuu ya Gombe, Kinshansa akituhumiwa kusafirisha kiholela, kumiliki isivyo halali madini ya almasi na kujaribu kuwahonga maafisa wa Jamhuri ya Kongo.

Awali mwendesha mashtaka wa serikali alitaka Kumar ahukumiwe kwenda jela miaka 17 pamoja kulipa faini ya dola milioni 500 kwa hasara ambayo ameisababishia serikali ya Kongo.

Lakini hakimu wa kesi hiyo aliamua Kumar atumikie kifungo cha miezi sita jela pamoja na kulipa faini ya dola 100,000 huku madini hayo ya almasi yakitaifishwa kwa serikali.

Madini hayo yalipofanyiwa utafiti na wataalamu wa madini wa Jamhuri ya Kongo, yaligundulika kuwa na uzito wa karati 42,000 na yakiwa na thamani ya dola 500,000.

Wakili wa serikali alipinga hukumu iliyotolewa akisema haitoi funzo kwa wafanyabiashara wengine wanaouza almasi kimagendo na aliongeza kuwa anasubiria waziri wa sheria atoe malalamiko yake kwa hukumu hiyo.

Kumar alikamatwa tarehe 10 mwezi huu kwenye uwanja wa ndege wa Kinshansa akijaribu kuyasafirisha madini hayo aliyoyaficha kwenye begi lake akiyapeleka India.

Wakati wa taratibu za ulinzi uwanjani hapo, polisi mwanamke wa uwanja wa ndege alikuta mfuko wa Rambo ndani ya begi la Kumar ukiwa na madini ya almasi ambayo yalikuwa hayana hati husika za kuyasafirisha nje ya nchi hiyo.

Katika utetezi wake Kumar alijitetea kuwa alikuwa hana nia ya kusafirisha madini ya almasi akiendelea kusema kuwa alikuwa hajui kuwa amenunua almasi yeye alijua amenunua vito kwa ajili ya kutengenezea shanga na vidani vya wanawake.

source.nifahamishe.com

Miujiza ya Kijana Aliyefariki Yawapagawisha Wengi

Wednesday, December 23, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Mamia ya watu wanamiminika kwenye nyumba ya kijana mmoja nchini Australia ambaye muda mfupi baada ya kufariki kuta za nyumba yake zimeanza kutoa mafuta ya ajabu ambayo yanadaiwa kuwatibu watu magonjwa yao.
Wazazi wa kijana Mike Tannous aliyefariki miaka mitatu iliyopita wanadai kuwa kijana wao amechaguliwa na mungu kuwa mtawa wa kwanza wa kiume wa Australia.

Mike alifariki mwezi septemba mwaka 2006 akiwa na umri wa miaka 17 kutokana na ajali ya gari lakini wiki chache baadae kuta za chumba chake zilianza kutoa mafuta ya ajabu ambayo yanadaiwa kuwatibu mamia ya watu magonjwa yao.

Wazazi wake Mike, George na Lina wanaoishi katika kitongoji cha Guildford katika jiji la Sydney wamedai kuwa kijana wao ni mjumbe wa mungu na ameishawatibu watu wengi sana kwa miujiza yake.

Mafuta yanayomiminika kwenye kuta za nyumba yake yamefanyiwa uchunguzi wa kisayansi na wataalamu mbali mbali lakini bado hayajagundulika ni mafuta ya aina gani.

Mamia ya watu wamekuwa wakimiminika kwenye nyumba yao kuyaona na kusali wakiomba yawatibu magonjwa yao.
“Mtoto wetu ni mtawa, anazungumza nasi na anazungumza na watu kwa njia hii”, alisema baba wa kijana huyo.

“Mwaka jana mwanamke mmoja anayeishi karibu na nyumba yetu aliambiwa na madaktari hataweza kupata mtoto wa tatu kwa njia yoyote ile, alikuja hapa na kuanza kusali… mwezi mmoja baadae alirudi na boksi la biskuti akitamba kuwa amepata ujauzito”, alisema shangazi yake Mike, Susan Sawan.

Mamia ya watu wamekuwa wakimiminika kila siku kwenye nyumba hiyo na hivi sasa si kuta za chumba chake pekee zinazovuja mafuta bali kuta zote za nyumba hiyo ya vyumba vitatu mpaka kwenye picha ya Mike ukutani.

“Mwishoni mwa wiki watu huja toka sehemu mbali mbali na kutufanya tufunge mtaa, wanataka kushuhudia miujiza”, alisema baba wa kijana huyo aliyefariki.

Kutokana na habari za miujiza ya tiba ya mafuta ya kuta za nyumba hiyo kusambaa, mamia ya watu kutokana nchi mbali mbali duniani nao wamekuwa wakimiminika Austalia kushuhudia mafuta hayo.

Wazazi wa Mike wamesema kuwa wao hawakusanyi mchango wowote toka kwa watu wanaofika kwenye nyumba yao wanachopenda wao ni kuona watu wakipatiwa tiba kutokana na miujiza ya mtoto wao.

Familia hiyo imekuwa ikiwajibu watu wasioamini wanaotilishia shaka miujiza ya mafuta hayo kwa kuwaambia “Njoo na ushuhudie mwenyewe”.

source.nifamishe.com

Wanafunzi Wanyonyana Sehemu za Siri Darasani

Wednesday, December 23, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Wanafunzi wawili wa shule moja ya msingi ya nchini Marekani wamesimamishwa masomo kwa kipindi kisichojulikana baada ya kunyonyana sehemu za siri darasani mbele ya wanafunzi wenzao huku mwalimu ambaye alikuwa darasani wakati huo akishuhudia naye amenyang’anywa leseni yake ya ualimu.
Wanafunzi hao wa darasa la nane katika shule moja ya msingi katika mji wa Houston, Texas nchini Marekani wamesimamishwa shule kwa kipindi kisichojulikana baada ya kupatikana na hatia ya kufanya kitendo nje ya maadili ya kishule.

Wanafunzi hao walinyonyana sehemu za siri mbele ya kundi la wanafunzi wenzao huku mwalimu mmoja akiwa ndani ya darasa hilo hilo akiendelea kuwaelekeza masomo wanafunzi wengine.

Taarifa zilizotolewa zilisema kwamba baadhi ya wanafunzi walitengeneza duara kumziba mwalimu wao asione kinachoendelea wakati wanafunzi hao wa shule ya msingi wakinyonyana sehemu za siri huku wanafunzi wengi wakishuhudia kitendo hicho.

Baada ya tukio hilo, mmoja wa wanafunzi alipeleka taarifa kwa mwalimu mkuu wa shule hiyo ambaye alipeleka taarifa polisi.

Wanafunzi hao walikamatwa na kuwekwa mahabusu katika jela za watoto na walifunguliwa mashtaka mahakamani ya kuharibu utulivu darasani na kufanya kitendo kinyume na maadili mbele ya watu.

Wanafunzi hao ambao majina yao hayakutajwa kutokana na sababu za kisheria, walikiri makosa yao katika mahakama ya watoto ya Houston.

Mwanafunzi wa kike alikabidhiwa kwa wazazi wake wakati uchunguzi wa suala hilo ukiendelea huku mwanafunzi wa kiume akiendelea kushikiliwa na polisi.

Mwalimu aliyekuwa darasani wakati huo ambaye alishindwa kuzuia wanafunzi hao wasiendelee kufanya kitendo hicho, amenyang’anywa leseni yake ya ualimu.

source.nifahamishe.com

Mtanzania Auliwa Kwa Kuchomwa Kisu Uingereza

Wednesday, December 23, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Kijana wa Kitanzania mwenye umri wa miaka 18 aliyekuwa akiishi na kusoma nchini Uingereza ameuliwa kwa kuchomwa kisu na kijana wa Kiingereza mwenye umri wa miaka 15 aliyekasirishwa na maoni mabaya aliyoyatoa kwenye ukurasa wake wa Facebook.
Kijana wa Kitanzania Salum Kombo aliyekuwa akiishi na kusoma nchini Uingereza ameuliwa na rafiki yake wa karibu kijana wa Kiingereza mwenye umri wa miaka 15 aliyekasirishwa na maoni ambayo Salum aliyaandika kwenye ukurasa wake wa Facebook.

Salum aliuliwa kwa kuchomwa na kisu shingoni na begani kwenye uwanja wa basketball uliopo karibu na nyumbani kwao.

Taarifa zilizopatikana zilisema kwamba rafiki huyo wa Salum aliandika maoni kwenye ukurasa wake wa Facebook akionyesha hasira zake kwa kutoalikwa katika party iliyoandaliwa na rafiki zake.

Salum alijibu maoni hayo kwa kuandika maoni ya kumkashifu rafiki yake huyo ambaye kutokana na kukasirishwa kwake alitishia kumuua lakini hakuna mtu aliyetilia maanani vitisho hivyo.

Salum ambaye alikuwa akisomea Sanaa kwenye chuo cha Tower Hamlets College jijini London alikutana na rafiki yake huyo kwenye uwanja wa basketball uliopo karibu na nyumbani kwao ambapo bila kutarajia rafiki yake huyo alimshambulia kwa kumchoma na kisu mabegani na shingoni.

Katika tukio lililotokea siku ya jumapili jioni mbele ya marafiki zake, Salum alijaribu kujikongoja kuelekea kwao huku damu kibao zikimtiririka lakini hakufika mbali na alifariki dakika chache baadae wakati akipewa huduma ya kwanza kwenye eneo la tukio hilo.

Muuaji wake amekamatwa na alipandishwa kizimbani jana jijini London.

Salum aliwasili Uingereza miaka saba iliyopita na alikuwa akiishi na shangazi yake jijini London.

Salum amekuwa kijana wa 13 ndani ya mwaka huu kuuliwa kutokana na mashambulizi ya visu jijini London.

source.nifahamishe.com
om

MWanamke afia gesti kuitatanishi, Kimara

Thursday, December 17, 2009 / Posted by ishak / comments (0)

MWANAMKE ambaye hakuweza kufahamika jina wala makazi yake anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25 na 30, amekutwa amekufa katika nyumba ya kulala wageni iitwayo Marangu huko Kimara jijini Dar es salaam.
Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye, amesema tukio hilo limetokea jana majira ya saa 5 asubuhi, huko maeneo ya Kimara Mwisho.


Alisema maiti ya mwnwamke huyo ilikutwa ikiwa imelala kitandani huku mdomoni ikiwa inatoka mapovu na haikuweza kufahamika mara moja chanzo cha kifo hicho.


Alisema kuwa, mwanamke huyo alifika katika gesti hiyo Desemba 13, majira ya saa 4 asubuhi na alipanga katika nyumba hiyo akiwa na kijana mmoja aliyejitambulisha kwa jina la James Joshua, mkazi wa jijini Dar es Salaam.


Katika maelezo yaliyopatikana katika nyumba hiyo ilidaiwa kuwa, kwa mara ya mwisho mwanamume aliyeuingia gesti na dada huyo aliaga kwa mhudumu mmoja alyekuwa zamukuwa anakwenda kutafuta chakula aina ya chipsi na hakurejea tena.


Amesema baada ya wahudumu kutaka kuingia katika chumba hicho kwa nia ya kufanya usafi, ndipo walipobaini dada huyo kuwa aklikuwa ameshakufa.

Maiti imehifadhiwa Hospitali ya Mwananyamala na polisi wanaendelea kumsaka kijana huyo kwa udi na uvumba.


source.nifahmishe.com

Aua Watu Wawili Ili Ahukumiwe Kunyongwa

Thursday, December 17, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja wa nchini China ambaye alikuwa na nia ya kujiua baada ya kushindwa kupata kazi kwa muda mrefu, amewaua watu wawili ili ahukumiwe kunyongwa.
Mwanaume huyo alikuwa na nia ya kujiua lakini alikuwa hana ujasiri wa kuitoa roho yake mwenyewe. Aliamua kuwaua watu wawili ili ahukumiwe adhabu ya kunyongwa.

Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 20 ambaye alitajwa kwa jina moja tu la Bin, alichukua uamuzi huo kutokana na hali ngumu ya maisha aliyokuwa nayo baada ya kushindwa kupata kazi kwa muda mrefu.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya mji wa Jiangmen katika jimbo la Guangdong, Bin aliwaua watu wawili kwa kuwanyonga ili ahukumiwe adhabu ya kifo.

"Kwa muda mrefu sina kazi, sina uwezo wa kujiua mwenyewe, nimefanya mauaji ili nihukumiwe kunyongwa", alisema Bin.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na polisi, Bin hana uhusiano wowote na wala alikuwa hawajui watu aliowaua.

source.nifahmishe.com

Mtoto wa Miaka 10 Apandishwa Kizimbani Kwa Ubakaji

Thursday, December 17, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Watoto wawili wa kiume wa nchini Uingereza wenye umri wa miaka 10 wamepandishwa kizimbani wakituhumiwa kumbaka mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 8.
Watoto hao wakisindikizwa na ndugu zao walipandishwa kizimbani katika mahakama ya Uxbridge, magharibi mwa mji wa London, wakikabiliwa na kesi ya ubakaji.

Katika tukio hilo lililotokea oktoba 27 mwaka huu, watoto hao wanatuhumiwa kushirikiana kumbaka mtoto wa kike mwenye umri wa miaka minane wakati walipokuwa wakicheza kwenye bustani ya Hayes, iliyopo magharibi mwa London.

Watoto hao kila mmoja amefunguliwa mashtaka mawili ya ubakaji.

Waliachiwa kwa dhamana wakati uchunguzi wa kesi yao ukiendelea na watapandishwa tena kizimbani tarehe 28 mwezi ujao.

Kutokana na umri wa watuhumiwa hao, vyombo vya habari vimewekewa masharti na mahakama katika kuripoti tukio hilo.

Vyanzo vya mahakama vimeelezea kushtushwa na kesi hii ya ubakaji kutokana na umri mdogo sana wa watuhumiwa.

Kwa mujibu wa sheria za Uingereza umri wa mtoto kufunguliwa mashtaka ya jinai ni miaka 10. Nchini Scotland sheria zinaruhusu kuwafunguliwa mashtaka watoto wenye umri wa miaka minane. Umri huo ndio mdogo kulinganisha na nchi zingine za barani ulaya.

source.nifahmishe.com

Mwanamke Ajifungua Mtoto Gym Akinyanyua Vyuma

Thursday, December 17, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamke aliyeiwakilisha nchi ya Chile kwenye mashindano ya Olimpiki ya kunyanyua vitu vizito, alikuwa hajui kama ana mimba, amejifungua mtoto ndani ya gym wakati akifanya mazoezi ya kunyanyua vyuma.
Elizabeth Poblete, 22, mwanamichezo aliyeiwakilisha Chile kwenye mashindano ya kunyanyua vitu vizito kwenye olimpiki mwaka jana nchini China, amejifungua mtoto ndani ya gym alipokuwa akifanya mazoezi ya kunyanyua vitu vizito.

Elizabeth alikuwa hajui kama ana mimba na alijifungua mtoto huyo kwenye gym iliyopo kwenye mji wa Sao Paulo nchini Brazili alikoweka makazi yake.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na tovuti ya habari ya Globo.com, Elizabeth alijifungua mtoto wa kiume ambaye amempa jina la Eric Jose.

Akiongelea tukio hilo kocha wake wa gym, Horacio Reis, alisema kuwa alikuwa hajui kama Elizabeth alikuwa na mimba kwani wiki iliyopita aliweza kushiriki na kushinda kwenye mashindano ya kubeba vyuma yaliyofanyika nchini Chile.

"Mashindano yalimalizika salama na alishinda", alisema kocha wake.

Kwa mahesabu ya madaktari, Elizabeth alikuwa na mimba ya miezi sita lakini kutokana na lishe na mazoezi aliyokuwa akifanya, mzunguko wake wa damu za hedhi ulikuwa hauna mpangilio maalumu hivyo kumfanya asigundue kuwa ana mimba.

Elizabeth aliiwakilisha Chile kwenye mashindano ya olimpiki yaliyofanyika Beijing, China mwaka jana.

Katika miezi ya karibuni, alikuwa kwenye mazoezi makali na lishe ya nguvu ili kuupandisha uzito wake kutoka kilo 75 hadi 85.


source.nifahamishe.
com

Ajali Yasababisha Awe na Hamu ya Mapenzi Wakati Wote

Thursday, December 17, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamke mmoja wa nchini Marekani maisha yake yamebadilika baada ya kupata ajali ambayo imesababisha awe na hamu ya kufanya mapenzi muda wote. Msuguano wa nguo na mwili wake husababisha awe kwenye kilele cha mapenzi bila hata kuguswa na mwanaume yoyote.
Kutokana na ajali ya gari ambayo ilisababisha madhara kwenye mishipa ya fahamu inayokatiza kwenye nyonga yake, Joleen Baughman mwenye umri wa miaka 39 amekuwa akikabiliwa na hali ambayo humtesa masaa 24 ya kila siku.

Ajali hiyo iliyotokea miaka miwili iliyopita, ilisababisha mshipa wa fahamu uliopo kwenye nyonga ambao husimamia matamanio ya kimapenzi ya binadamu uwe kama umeachiliwa kufanya kazi muda wote.

Wakati wote Joleen hutamani kufanya mapenzi bila hata kutosheka.

Kutokana na hali hiyo, kitendo cha kukaa kwenye kiti, kuinama na hata kutembea ndani ya chumba chake husababisha mambo yawe si mambo kwenye nyeti zake bila hata kuguswa na mtu yoyote sehemu hizo.

Joleen ambaye ni mama wa watoto wawili mkazi wa New Mexico, Marekani alisema "Ni hali ambayo nashindwa kujizuia, hata msuguano wa nguo nilizovaa na mwili wangu husababisha niwe kwenye hamu kubwa sana ya kufanya mapenzi".

Joleen ambaye anaishi na mumewe Brian, 39, na watoto wao wawili anakabiliwa na ugonjwa unaowapata watu wachache sana unaoitwa "Restless Genital Syndrome".

Joleen alipata ajali mwezi aprili mwaka 2007 wakati alipokuwa kwenye gari na mumewe na gari lao kugongana uso kwa uso na gari la mwanaume aliyekuwa amelewa madawa ya kulevya.

Joleen alilazwa hospitali wiki kadhaa baada ya kufanyiwa operesheni ya ubongo na uti wake wa mgongo ambao nao ulivunjika katika ajali hiyo.

Alipona taratibu na kuruhusiwa kurudi nyumbani kwake lakini baada ya miezi sita madhara ya ajali hiyo yalianza kujitokeza.

Joleen ambaye awali alikuwa sio mpenzi sana wa kufanya mapenzi, alianza kushikwa na hamu ya ajabu ya ngono muda wote.

Awali yeye na mumewe wa ndoa ya miaka 20 walifurahia hali hiyo kwa kuwa mumewe alikuwa akipenda sana kufanya tendo la ndoa.

"Brian alikuwa na furaha kwamba kwa mara ya kwanza katika ndoa yetu mimi ndio nalazimisha kufanya mapenzi muda wote", alisema Joleen.

"Ndani ya siku moja kwa mfano tungefanya mara ya kwanza, tuliporudia mara ya pili ndio kwanza hamu yangu ya kimapenzi huanza kuongezeka, tunapoenda raundi ya tatu huwa nahisi maumivu lakini nakuwa na hamu kuliko mwanzo".

Baada ya kugundua kuwa kufanya mapenzi mara nyingi hakutatibu tatizo lake, Joleen alianza kutafuta tiba ya tatizo lake.

Alikata tamaa baada ya madaktari kumwambia kuwa tatizo lake si la kisaikolojia bali linatokana na mshipa wa fahamu unaoitwa pudendal uliopo kwenye nyonga karibu na sehemu za siri.

Kutokana na ugonjwa huo kutokuwa na tiba maalumu, Joleen bado anaendelea kusumbuliwa na tatizo hilo hadi leo.

source.nifahmishe.com

Mapenzi! Mapenzi! Aifukua Maiti ya Mkewe na Kulala Nayo

Tuesday, December 01, 2009 / Posted by ishak / comments (0)

Mwanaume mmoja wa nchini Vietnam ambaye alikuwa na huzuni ya kuondokewa na mkewe, alifukua kaburi la mkewe na kuichukua maiti ya mkewe na kuanza kulala nayo kitanda kimoja kwa kipindi cha miaka mitano.
Le Van aligubikwa na huzuni kubwa wakati mkewe alipofariki mwaka 2003 kiasi cha kwamba alianza kulala juu ya kaburi lake katika mji wa Quang Nam uliopo ukanda wa kati wa Vietnam.

Gazeti la Vietnamnet liliripoti kuwa Van aliendelea kulala juu ya kaburi la mkewe usiku kwa kipindi cha miezi 20 mpaka alipoanza kuugua kutokana na hali ya hewa ya baridi.

Ili kujikinga na baridi, Van aliamua kutengeneza handaki lililoenda kwenye jeneza lake na kuanza kulala pembeni ya maiti yake.

Watoto wa Van waliligundua handaki hilo na waliamua kumzuia Van kulitembelea kaburi la mkewe.

Mwezi novemba mwaka 2004, Van alilifukua kaburi la mkewe na kuichukua maiti ya mkewe hadi nyumbani kwake.

Van alitumia udongo mfinyazi kuizunguka mifupa ya maiti ya mkewe na kisha aliivalisha maiti hiyo nguo za kike na kisha kuipaka vipodozi.

Van mwenye umri wa miaka 55, baba wa watoto saba, alianza kulala pembeni ya maiti ya mkewe akiikumbatia kuanzia wakati huo hadi leo.

Picha zinazomuonesha Van akiwa pembeni ya maiti ya mkewe zilichapishwa kwenye gazeti la Vietnamnet, ikiwemo picha moja ambayo iliionyesha mifupa ya mkono wa mkewe ikiwa imezungushiwa udongo.

"Mimi ni mtu ninayependa kufanya vitu tofauti.. mimi si mtu wa kawaida", Van alisikika akiliambia gazeti hilo.


source.nifahamishe.com

Auliwa na Mumewe Akisherehekea Kupewa Talaka

Tuesday, December 01, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Mama wa watoto wawili wa nchini Uingereza ameuliwa na mumewe baada ya kuandaa sherehe ya kusherehekea kupewa talaka.
Katrina Jones mwenye umri wa miaka 34 aliuwa na mumewe kwa kuchomwa chomwa na kisu masaa machache kabla ya kuanza kwa sherehe aliyoiandaa kusherehekea kupewa talaka.

Mwili wa Katrina ulikutwa ukiwa katika dimbwi la damu ukiwa na majeraha kibao ya kuchomwa na kisu asubuhi ya siku ya jumamosi masaa machache kabla ya wageni waalikwa kuanza kuwasili kwenye sherehe aliyoiandaa "Divorce Party" kusherehea kuvunjika kwa ndoa yake na mumewe.

Mume wake aliyejulikana kwa jina la Brian Jones mwenye umri wa miaka 63 alikamatwa na kushikiliwa na polisi na baadae kufunguliwa mashtaka ya mauaji.

Majirani zake walisema kuwa ndoa ya miaka 9 ya Katrina na Brian ilivunjika mwezi februari mwaka huu.

Siku ya ijumaa Katrina aliweka mabango kwenye madirisha ya nyumba yake katika kitongoji cha Marske, Middlesbrough akiwaalika watu katika sherehe yake ya kuvunjika kwa ndoa yake.

Lakini aliuliwa na mumewe siku iliyofuatia kabla hata ya kuanza kwa sherehe hiyo.

Majirani walimuelezea Brian kuwa ni mtu mwenye vurugu kiasi cha kuogopwa na majirani zake.

Majirani walisema kuwa Katrina aliamua kuachana na mumewe baada ya mapenzi yake kwa mumewe kuisha kutokana na tabia zake.

"Ilikuwa ni vigumu kwake kukubali kuwa ndoa yake na Katrina imevunjika", alisema mmoja wa majirani zake akielezea sababu iliyopelekea Brian kumuua mkewe.

Katrina alikuwa ni mke wa tatu wa Brian baada ya ndoa zake mbili za mwanzo kuvunjika.


source.nifahamishe.com

Matumaini ya Mkenya Kumuoa Mtoto wa Clinton Yaota Mbawa

Tuesday, December 01, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Chelsea Clinton, mtoto wa rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton amekubali posa ya mpenzi wake wa muda mrefu na hivyo kuyafuta kabisa matumaini ya raia wa Kenya ambaye alituma posa ya kumuoa akiahidi kutoa ng'ombe 20 na mbuzi 40.
Awali Mkenya huyo Godwin Kipkemoi Chepkurgor mwenye umri wa miaka 40 alituma posa ya kumuoa Chelsea Clinton, binti wa rais wa zamani wa Marekani, Bill Clinton mwaka 2000 na aliahidi kutoa ng'ombe 20 na mbuzi 40 kama mahari.

Kipkemoi alikumbushia nia yake ya kumuoa Chelsea, wakati mama yake Chelsea ambaye pia ni waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Hillary Clinton, alipofanya ziara yake nchini Kenya mwaka huu miezi michache iliyopita.

Hillary alimjibu Kipkemoi kuwa Chelsea ni mtu mzima na ana maamuzi yake lakini atamfikishia ujumbe huo.

Matumaini ya Kipkemoi kumuoa Chelsea yamefutika baada ya Chelsea kukubali kuchumbiwa na mpenzi wake wa muda mrefu Marc Mezvinsky.

Mezvinsky ambaye ni mfanyakazi wa benki ya Goldman Sachs alikuwa rafiki wa karibu wa Chelsea tangia utotoni.

Msemaji wa familia ya Clinton alitoa taarifa wiki hii kuwa Chelsea na Mezvinsky walivalishana pete ya uchumba wiki iliyopita.

Kama Chelsea angekubali kuolewa na Kipkemoi angekuwa mke wa pili wa Kipemoi ambaye alifunga ndoa na mwanamke mwingine raia wa Kenya mwaka 2006 baada ya kusubiria majibu ya posa yake ya kumuoa Chelsea kwa miaka sita.

Kipkemoi alidai kuwa mkewe yuko radhi kushea nyumba moja Chelsea Clinton.

Kwa mujibu wa sheria za Kenya, mwanaume anaruhusiwa kuoa zaidi ya mke mmoja.


source.nifahamishe.com

Rihanna Akanusha Kumhonga Penzi Jay-Z

Wednesday, November 25, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Nyota wa muziki wa R&B wa Marekani Rihanna amekanusha uvumi uliozagaa nchini Barbados alikozaliwa kuwa alimhonga penzi mkongwe wa hip hop Jay-Z ili apate umaarufu alio nao sasa.
Nyota wa muziki wa R&B wa Marekani aliyetamba na nyimbo yake ya "Umbrella" ameelezea kuchukizwa na uvumi uliozagaa wakati alipoanza kuwika kwenye anga ya muziki kuwa alimhonga penzi Jay-Z ili ampe tafu kwenye masuala ya kimuziki.

Kipaji cha muziki cha Rihanna kilivumbuliwa kwenye visiwa vya Barbados na Jay-Z ambaye aliamua kumpa tafu Rihanna kuandaa albamu yake ya kwanza.

Lakini Rihanna anasema kuwa uvumi ulizagaa kila kona kwenye visiwa hivyo kuwa alimpa uroda Jay-Z ili ampe tafu kimuziki.

Rihanna anasema kuwa hata marafiki zake wa karibu waliamini kuwa alilala na Jay-Z ili apewe tafu.

Rihanna amekanusha uvumi huo na kusema kuwa hakuwahi kuwa na uhusiano wowote wa kimapenzi na Jay-Z.

"Uvumi huu ulinifanya nijisikie vibaya wakati wote na nilishindwa hata kumuangalia machoni Jay-Z", alisema Rihanna.

"Siku moja Jay-Z aliniita na kuniambia nisisikilize watu wanachovumisha, nisiishi kwa kufuatisha maneno ya watu", alisema Rihanna.


source.nifahamishe.com

BUSTA RYMES ALIVYOKAMUA NDANI YA FIESTA 2009

Sunday, November 22, 2009 / Posted by ishak / comments (0)







Busta Rymes alikonga nyoyo ya washabiki katika fiesta one pamoja na vijana wake aliokuja nao
pia Chid Benz aliwasha moto kilivyo kwa mashabiki waliofurika kama nyuki

Urembo Inapotumbukia Nyongo

Friday, November 20, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanafunzi mmoja wa kike wa nchini Uingereza ameharibika sura yake kabisa kiasi cha kufanana na UFO (viumbe vinavyosemekana vinaishi angani) baada ya kutumia dawa ya kuzibadilisha rangi nywele zake ziwe nyeusi.
Abigail Colbourne mwenye umri wa miaka 15, alitumia dawa za kupaka za kubadilisha rangi ya nywele kuwa nyeusi za kampuni ya Clairol ili kuzifanya nywele zake ziwe nyeusi lakini ghafla sura yake ilianza kuvimba na macho yake yalivimba kiasi cha kushindwa kuona.

Sura yake iliharibika kabisa kiasi cha kushindwa kutambulika.

Akiongea na gazeti la The Sun la Uingereza Abigail alisema "Macho yangu yalifunga kutokana na jinsi yalivyovimba na kichwa changu pia kilivimba... nilikuwa natisha sana".

Abigail ambaye ni mkazi wa London alisema kwamba alishindwa kufanya vipimo vya aleji kabla ya kujipaka dawa hizo kama ilivyoshauriwa kwenye paketi ya dawa hizo.

Aliwahishwa hospitali ambako alipatiwa matibabu na uvimbe huo kupungua kidogo. Bado anaendelea na matibabu ya kuirudisha sura yake katika hali yake ya awali.

Mama yake Abigail, Joanna Leech alisema kuwa tukio hilo la kusikitisha lililompata mwanae liwe fundisho kwa wengine wanaotumia dawa kama hizo.

by nifahamishe.com

TOVUTI YA WATU BOMBAA PEKEE

Thursday, November 19, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Tovuti ya watu wazuri pekee yake imekuwa ikipata wanachama wengi hadi sasa ina wanachama 180000 ila imekuwa ikisababisha chembe ya ubaguzi kwa watu wasio na mvuto,hebu tembelea hii mdau

www.beautifulpeople.com

Kikwete anena kuhusu adhabu ya vifo

Thursday, November 19, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Rais Kikwete abadilisha hukumu ya vifo katika kesi 75 ambazo hukumu yake imekuwa kifungo cha maisha

Busta Rymes atawasha moto katika fiesta Dar

Thursday, November 19, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


mwana muziki machachari kwa kufloo atawasha moto katika fiesta ya tarehe 21 novemba,sijui itakuaje wadau nadhani patakuwa hapatoshi

AKON APATA SHAVU KATIKA UFUNGUZI WA KUMBE LA DUNIA

Thursday, November 19, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Akon atapiga shoo ya ufunguzi wa kumbe la dunia kule kwa babu south africa

KOMBE LA DUNIA LILIPOWASILI DAR

Thursday, November 19, 2009 / Posted by ishak / comments (0)

kombe la mabingwa wa barclays league lilivyotinga dar

Monday, November 16, 2009 / Posted by ishak / comments (0)




watu mbalimbali walivyopiga picha na kombe hilo

MAISHA CLUB JINSI ILIVYOTEKETEA KWA MOTO

Monday, November 16, 2009 / Posted by ishak / comments (0)






Maisha club ilivyoteketea kwa moto,sehemu ya ndani na nje kama jinsi inavyoonekana

Unga Unawamaliza Wasanii wa Bongo Flava

Sunday, November 08, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Muziki wa kizazi kipya Bongo Flava uko hatarini kutokana na kwamba mastaa wake wengi ambao wamewahi kutamba katika fani hiyo wanaanza kupotea mmoja mmoja baada ya kupata pesa na kujiingiza kwenye matumizi ya madawa ya kulevya.
Unga unaimeng’enya Bongo Flava
Mambo hayapo ok, Bongo Flava inazidi kumeng’enywa na nguvu kazi yake inapungua. Hapa ni gumzo kuwa vijana wengi wapo kwenye skendo ya kutumia dawa za kulevya.

Kuna maswali magumu; Kwanini baadhi ya wasanii wana-shine kidogo, wanakubalika kitaa na kiasi fulani maisha yao kuwa bora lakini ghafla tu madogo wanaonekana kitaa wamechoka na afya zimekuwa dhaifu.

Madai ya msingi ni matumizi ya dawa za kulevya a.k.a unga, kwamba madogo wengi wakishakubalika kitaa kwa njia moja au nyingine hujiingiza kwenye matumizi ya unga, wanabwia na wengine wanajidunga kabisa.

Its dangerous! The only gent on kundi marehemu la Wakilisha, Langa Kileo anaweza kuwa mfano hai, baada ya kukiri kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM Ijumaa iliyopita kuwa alikuwa anabwia unga lakini sasa amestop. Langa alisema kuwa alikuwa mbwiaji mzuri wa Cocktail kabla ya hivi karibuni kuugua typhoid, hivyo kukosa access ya kupata unga.

Alisema, alianza kama utani lakini baadaye alizidiwa na akawa hawezi kuacha, ingawa sasa hivi anamshukuru Mungu kwamba yamepita. Katika hilo, Langa alieleza kwamba angalau sasa anajisikia nafuu na afya imeanza kurejea. Hiyo ni kauli ya Langa kupitia session ya Crazy Friday, lakini ukweli ni kuwa madogo kibao wapo kwenye skendo ya kubwia.

Albert Mangwea ‘Ngwair’, Heri Samir ‘Blu’ Mark II B a.k.a Simba ni kati ya majina ambayo yanatajwa kwenye orodha ya wanaodaiwa kubwia unga. Hayo ni majina yanayotajwa lakini nyuma ya pazia ni wengi na hii inasababisha kizazi kipya kisiwe na afya standard. Madogo wanasimama vizuri lakini baadaye wanakuwa dhoofu l’hali. Hii ni hatari na sisi kama wadau tunalaani vikali matumizi ya dawa za kulevya.

source.nifahamishe

Jambazi Anapowatumia Polisi Picha Yake...

Sunday, November 08, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Jambazi anayetafutwa na polisi kila kona nchini Uingereza amewatumia polisi picha yake mpya aliyopiga akiwa mbele ya gari ya polisi baada ya kuchukizwa na picha yake ambayo polisi waliitoa kwenye magazeti wakiomba wananchi wawasaidie kumnasa.
Jambazi Matthew Maynard mwenye umri wa miaka 23 hakuipenda picha yake iliyotolewa kwenye magazeti na aliamua kuwatumia polisi picha yake mpya aliyopiga akiwa mbele ya gari la polisi.

Polisi katika mji wa Swansea walitoa tangazo la kutafutwa kwa Matthew katika gazeti la Evening Post la mji huo. Tangazo hilo liliambatana na picha yake ndogo inayoonyesha sura yake.

Baada ya picha hiyo kuchapishwa kwenye gazeti hilo, Matthew ambaye pamoja na wenzake wanne wanatafutwa na polisi kwa makosa ya ujambazi, alipiga simu kwenye ofisi ya gazeti hilo akisema kuwa hajaipenda picha yake iliyotolewa kwenye gazeti hilo na aliwaahidi atawatumia picha nyingine waiweke kwenye gazeti lao.

Wakati waandishi wa gazeti hilo wakiwa hawaamini kama kweli atawatumia picha yake, Matthew alitumia simu yake kuwatumia picha yake aliyopiga akiwa mbele ya gari la polisi akiwa amevaa jaketi linalofanana na majaketi wanayopenda kuvaa mapolisi.

Picha yake hiyo ilitolewa juzi kwenye ukurasa wa mbele wa gazeti la Evening Post.

Jana polisi wa Swansea walimshukuru Matthew kwa kuwasaidia polisi katika harakati zao za kumtia mbaroni.

"Anajiona mjanja sana kwa kujionyesha namna hii, tutamnasa muda si mrefu", alisema afisa mmoja wa polisi.

"Watu wote wa Swansea wanajua sasa jinsi alivyo na watatupa taarifa zitakazofanikisha kukamatwa kwake".

"Kama ana akili angejisalimisha mwenyewe polisi sasa kwakuwa hana pa kukimbilia tena", alimalizia kusema afisa huyo.

source.nifahamishe.com

CUF yamtambua Rais Karume, Maalim Seif Hamad Nusura Ashushiwe Kipigo

Sunday, November 08, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Katibu mkuu wa chama kikuu cha upinzani katika siasa za visiwa vya Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad alitangaza jana kumtambua rais Karume kama rais halali wa Zanzibar na kusababisha hasira toka kwa wafuasi wa CUF ambao almanusura wamshushie kipigo wakidai viongozi wa CUF wamewasaliti.
Akiongea katika mkutano wa hadhara katika uliofanyika kwenye viwanja vya Kibandamaiti, Maalim Seif Hamad alizomewa na kulazimika kushuka toka kwenye jukwaa akiwa chini ya ulinzi mkali baada ya kutangaza kuwa CUF imeamua kumtambua Rais Amani Abeid Karume.

Akiongea katika mkutano huo, Maalim Seif Hamad alisema kwamba baraza kuu la uongozi wa CUF limefanya kikao na kuamua kumtambua rais Amani Abeid Karume kama rais halali wa Zanzibar ili kumaliza msukosuko wa kisiasa katika visiwa hivyo.

Tamko hilo la Maalim Seif limefuatia kikao chake na rais Karume ndani ya ikulu ya Zanzibar na kisha kufuatiwa na mkutano wa baraza la kamati kuu ya chama hicho.

Maalim Seif alisema kuwa uamuzi huo ulikuwa ni mgumu kufanywa kwa vile chama hicho kimekuwa kikiibiwa kura zake katika uchaguzi kila uchaguzi unapofanyika visiwani humo.

Uamuzi huo wa Maalim Seif kumtambua rais Karume uliamsha hasira za wafuasi wa CUF ambao walianza kumzomea huku wakipiga kelele "hatukubali hatukubali".

Kutokana na vurugu iliyoanza kuzuka kwenye mkutano huo ambapo baadhi ya wafuasi wa CUF walianza kutembea kuelekea kwenye jukwaa hilo, ilibidi Maalim Seif alazimike kushuka jukwaani na kupewa ulinzi mkali kunusuru maisha yake na kwenda kukaa kwenye jukwaa la viongozi wa CUF.

Baada ya hapo mwenyekiti wa chama hicho Profesa Ibrahim Lipumba alipanda jukwaani kujaribu kuwatuliza wafuasi wenye hasira ambao waliwaona viongozi wao kama wasaliti na wengine kuangua kilio.

Hata hivyo hali haikutulia na wafuasi wa chama hicho walianza kupiga kelele za kuwataka viongozi wa chama hicho wajiuzulu.

Wafuasi hao walilalamika kuwa baadhi yao na ndugu zao wamepoteza maisha na wengine kuwa vilema kwa sababu ya kutetea siasa za chama hicho na matokeo yake chama hicho kimewasaliti.

Chama cha CUF kwa miaka kadhaa sasa katika chaguzi za mwaka 1995, 2000, na 2005 kimekuwa kikigoma kuitambua serikali na baadhi ya nyakati wajumbe wake wa baraza la wawakilishi waligoma kuingia vikaoni.

Miongoni mwa mazungumzo ya kutafuta muafaka yaliyofanyika mwezi Februari mwaka huu, yalikwama baada ya CUF kukataa kumtambua rais Karume kama rais halali wa Zanzibar na kwa upande wake rais Karume aligoma kuwachagua wajumbe wawili wa CUF kuingia katika baraza la wawakilishi kwa sababu hiyo hiyo.

Ukiwa ni mwaka mmoja tu umebakia kufanyika kwa uchaguzi mwingine mkuu visiwani humo, baadhi ya wataalamu wa siasa za Zanzibar wanadhani CUF itapita katika kipindi kigumu huku wengine wakiamini kuwa uamuzi wa kusamehe dhuluma wanzodai kufanyiwa unaweza kukifanya chama hicho kuwa imara zaidi visiwani humo.

source.nifahamishe.com

Obama Alikuwa Akikoroma Sana, Michelle Alikuwa Akichonga Sana

Friday, September 25, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Ndoa ya rais wa Marekani, Barack Obama na mkewe Michelle iliwahi kupitia misukosuko mikubwa ambayo ilitishia kuvunjika kwake. Miongoni mwa vitu vilivyokuwa vikisababisha kutokuelewana ni Obama kuvuta sana sigara na kukoroma sana usiku wakati Obama alikuwa akichukizwa na tabia ya Michelle kumsema sema sana kila wakati.
Wakati Obama alikuwa hapendi jinsi Michelle alivyokuwa akichonga sana na kumkosoa mara kwa mara, Michelle alikuwa akichukizwa na tabia ya Obama kukoroma sana wakati wa kulala na kuvuta sana sigara kiasi cha kwamba alikuwa akinuka sigara muda wote.

Mwaka 2007 wakati akifanya mahojiano na jarida la Glamour la Marekani, Michelle alisema kuwa Obama alikuwa ananuka sana sigara na kukoroma sana kiasi cha kwamba watoto wao walikuwa hawataki kulala naye.

Michelle pia alikuwa akichukizwa sana na Obama kujihusisha zaidi na siasa kuliko kuiangalia familia yake.

Mara kwa mara Michelle alimwambia Obama "Unajifikiria mwenyewe tu, sikuwahi kufikiria kwamba nitakuja kuilea familia peke yangu, sikuolewa kwaajili hii".

Michelle pia aliwahi kumwambia Obama wakati huo wakiwa na mtoto mmoja kwamba baada ya miaka minane ya ndoa yao, siku za ndoa yao zilikuwa zikihesabika na wakati wowote ingevunjika.

Kwa upande wake Obama alimwambia bibi yake Madelyn 'Toot' Dunham, ambaye alimlea alipokuwa Hawaii kwamba "Nampenda sana Michelle, lakini ni mkali sana na wakati wote ana hasira".

Maisha ya Obama na mkewe yameongelewa kwenye kitabu cha "Barack And Michelle: The Love Story " cha mwandishi wa habari wa Marekani na mtunzi wa vitabu, Christopher Andersen, ambacho kimeingia madukani wiki hii.

Historia ya Obama inaanzia Honolulu, Hawaii alikozaliwa kutokana na mama Mmarekani na baba 'Cha Pombe' (Mlevi sana) toka Kenya aliyekuwa mwanafunzi nchini Marekani.

Obama alilelewa na mama yake nchini Marekani na Indonesia wakati huo baba yake alirudi Kenya na kuoa mke mwingine.

Obama Alikutana na Michelle Robinson baada ya kumaliza mwaka wake wa kwanza kwenye chuo cha Harvard Law School, na kwenda kufanya field yake wakati wa likizo kwenye kampuni kubwa ya sheria inayoitwa Sidley Austin.

Michelle ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye kampuni hiyo ndiye aliyepewa majukumu ya kumsimamia Obama wakati wa field yake kwenye kampuni hiyo.

Obama alivutiwa na Michelle baada ya kutambulishwa na alimwambia rafiki yake baadae kwamba "Michelle ni mrembo sana, nitatumia uchawi wangu wote kumnasa".

Ili kumwingiza kwenye mitego yake, Obama alianza kumtumia Michelle maua na barua za kimapenzi pamoja kumpigia simu mara kwa mara mpaka alipokubali mwaliko wake baada ya kumsikia akitoa hotuba kwenye mkutano wa vijana weusi wa Marekani.

Hatimaye Obama alifanikiwa kumnasa Michelle na alifunga naye ndoa ilipofika oktoba 3 mwaka 1992.

Ndani ya miaka minne ya ndoa yao huku Obama akiwa amejikita zaidi kwenye siasa na kuchaguliwa kuwa seneta wa jimbo la Illinois, matatizo yalianza kujitokeza kwenye ndoa yao.

Michelle alikuwa akichukizwa na tabia ya Obama kutofanya usafi na kutozihifadhi vizuri soksi na chupi zake kwani baada ya kuzivua alikuwa akizitelekeza kwenye sakafu.

Michelle alichukizwa pia na tabia ya Obama kutofanya kazi yoyote ya nyumbani na kuacha mataulo yaliyolowa kwenye sakafu bafuni na pia kuacha vyombo vichafu kwenye sinki baada ya kula.

Hakuna kitu ambacho Michelle alikuwa akikichukia zaidi kama uvutaji wa sigara wa kupindukia wa Obama. Michelle alikuwa akilalamika nyumba yao ilikuwa ikinuka sigara na mazulia yao yote yalikuwa na matobo kutokana na moto wa sigara.

Wakati Michelle alikuwa akiingia kulala saa nne usiku ili awahi kuamka kuwahi kwenye kazi yake aliyokuwa akilipwa pesa nyingi sana, Obama alikuwa akiingia kitandani kulala mida ya saa nane usiku.

Mbali na kuingia kitandani kulala mida hiyo, Obama alikuwa akimsumbua Michelle kwa kukoroma sana.

Kuzaliwa kwa binti yao wa kwanza Malia, julai 4 mwaka 1998 hakukusaidia kuiimarisha ndoa hiyo badala yake kuliifanya ndoa hiyo iwe hatarini.

Obama alikuwa akitumia siku nne hadi tano akiwa mji mwingine kwenye bunge la Seneti na hali hiyo ilimfanya Michelle ajihisi ametelekezwa.

Michelle alifikiria kwamba Obama alikuwa akipoteza muda kwenye siasa badala ya kufanya kazi kama mwanasheria na kulipwa pesa nyingi zaidi.

Misuko suko kwenye ndoa ya Obama ilipungua wakati binti yake wa pili Natasha ambaye anajulikana zaidi kama Sasha alipopata ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo (Meningitis) mwaka 2001 wakati huo akiwa na umri wa miezi mitatu.

Sasha aliwahishwa hospitali na ilimbidi Obama na mkewe wapokezane kukaa naye hospitali kwa masaa 72 wakati alipolazwa kwa matibabu zaidi.

Baada ya hapo utulivu ulirudi kwenye ndoa yao na mambo yote yalikaa sawa baada ya Obama kushinda uchaguzi wa urais wa Marekani.

Hatimaye mwezi novemba mwaka jana katika mji wa Chicago familia ya Obama ilitambulishwa rasmi kuwa familia namba moja ya Marekani.

"Nisingesimama hapa bila ya msaada wa rafiki yangu wa miaka 16, nguzo ya familia yangu, mke wangu Michelle Obama" alisema Obama.

Hivi sasa familia ya Obama imesahau yaliyopita na imekuwa ikitolewa mifano kama mojawapo ya familia bora duniani.

Ronaldo wa Brazili Abambikiwa Mtoto

Thursday, September 24, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Nyota wa Brazili, Ronaldo de Lima ametakiwa na mahakama nchini Brazili afanye vipimo vya DNA ili kuondoa mzozo wa kubambikiwa mtoto na mwanamke raia wa Brazili anayeishi nchini Singapore.
Tangia Ronaldo aliporudi Brazili mwaka 2008 toka timu ya AC Milan ya Italia, amekuwa akikumbwa na maskendo mbali mbali kama vile kuanikwa kwenye magazeti baada ya kulala na mashoga hotelini na kisha kukataa kuwalipa baada ya huduma.

Safari hii Ronaldo amekumbwa na skendo jingine akidaiwa kuzaa na mwanamke raia wa Brazili anayeishi nchini Singapore na kisha kumkataa mtoto wake.

Ronaldo ambaye hivi sasa anaichezea timu kongwe ya Brazili ya Corinthians ametakiwa na mahakama nchini humo kufanya vipimo vya DNA ili kumaliza mzozo wa mwanamke anayedai Ronaldo ni baba wa mtoto wake mwenye umri wa miaka minne.

Taarifa toka jiji la Rio de Janeiro zinasema kwamba mwanamke huyo anayejulikana kama Michele Umrazu mwenye umri wa miaka 27, awali kabla ya kudai amezaa na Ronaldo alikuwa akidhania mtoto wake mwenye umri wa miaka minne ni wa mpenzi wake wa zamani raia wa Marekani.

Lakini baada ya vipimo vya DNA kufanyika na kugundulika kuwa mtoto huyo si wa huyo Mmarekani, Michele aligeuza kibao na kudai kuwa mtoto huyo ni wa Ronaldo.

"Nywele zake, macho yake mpaka pua vyote vinafanana na Ronaldo" alisema Michele.

Mama yake Michele alidai kwamba Ronaldo ambaye aliwahi kuchaguliwa kuwa mchezaji bora wa dunia mara tatu, alikutana na Michele kwa mara ya kwanza mwaka 2002 wakati wa kombe la dunia nchini Japan.

Walikutana tena mwezi wa nane mwaka 2004 ikiwa ni miezi tisa kabla ya kujifungua mtoto huyo.

Kutokana na Ronaldo kumkataa mtoto huyo, mzozo ulifika mahakamani na sasa mahakama imemtaka Ronaldo afanye vipimo vya DNA ili kumaliza mzozo huo.

Ronaldo ambaye alitimiza miaka 33 siku mbili zilizopita ana watoto wengine wawili Ronald, mwenye umri wa miaka tisa na Maria Sofia mwenye umri wa miezi tisa.

Ronaldo alithibitisha mwezi uliopita kuwa anatarajia mtoto wa tatu mwanzoni mwa mwaka ujao.

source.nifahamishe.com

Atumia Staili za Mike Tyson Kunyofoa Sikio la Mpenzi Wake

Thursday, September 24, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja wa nchini Ujerumani mwenye wivu wa ajabu baada ya mpenzi wake kuamua kuvunja uhusiano wao, kwanza alimshushia kipigo cha nguvu na kisha kutumia staili ya Mike Tyson kwa kumng'ata sikio lake na kunyofoa kipande cha sikio lake
Mike J. mfanyakazi wa kampuni ya ujenzi nchini Ujerumani alitumia staili ya wajina wake Mike Tyson kumng'ata sikio mpenzi wake aliyeamua kuvunja uhusiano wao.

Mike mwenye umri wa miaka 29 alipata hasira za ajabu baada ya mpenzi wake aliyetajwa kwa jina moja la Stephanie mwenye umri wa miaka 19, mwanafunzi wa sekondari nchini humo kumtamkia wazi kuwa hataki kuendelea na uhusiano wao wa kimapenzi wa miaka miwili.

"Mike ana wivu wa ajabu, muda mfupi baada ya kutamka maneno mazuri ya kimapenzi hubadilika ghafla na kuanza kunipiga, baada ya kubusiana naye huanza kuonyesha hasira zake", alisema Stephanie anayetoka mji wa Jessen.

"Baada ya kushauriana na rafiki zangu niliamua kuvunja uhusiano wetu" aliendelea kusema Stephanie.

Stephanie alisema kwamba baada ya kumtamkia wazi Mike kuwa hataki kuendelea na uhusiano wao wa kimapenzi, Mike hakuridhia na alimfuata siku hiyo hiyo nyumbani kwake mida ya usiku.

"Aliponigongea mlango nilidhani anakuja tuongee naye kuhusiana na uhusiano wetu lakini alipoingia ndani moja kwa moja alinirukia na kunipiga na kisha kuning'ata sikio na kunyofoa kipande cha sikio langu na kisha kukitema chini, kila sehemu ilijaa damu" alisema Stephanie.

Stephanie alidokeza kwamba alifanikiwa kukipata kipande cha sikio lake kilichonyofolewa lakini madaktari walishindwa kukiunga tena.

Mike alifikishwa mahakamani na alihukumiwa kifungo cha nje cha mwaka mmoja pamoja na kulipa faini ya euro 1600.

Mike alipinga hukumu hiyo na alidai atakata rufaa.

Tukio hili limekumbushia tukio la bingwa wa zamani wa ndondi Mike Tyson kumng'ata sikio Evander Holyfield wakati wa pambano lao lililofanyika juni 28 mwaka 1997.

source.nifahamishe.com

Berry black akamua uarabuni

Thursday, September 24, 2009 / Posted by ishak / comments (0)






source.djchoka

Aliyemrushia Bush Viatu Atoka Jela Akiwa Hana Meno Mawili

Wednesday, September 16, 2009 / Posted by ishak / comments (0)

Mtangazaji wa Iraq ambaye alitupwa jela baada ya kumrushia viatu vyake rais wa zamani wa Marekani George Bush wakati alipokuwa akiongea na waandishi wa habari nchini humo, ametoka jela jana huku akiwa amepoteza meno mawili kutokana na mkong'oto aliokuwa akipewa jela.
Muntazer al-Zaid mtangazaji wa televisheni ya Iraq ambaye alimfanya rais wa zamani wa Marekani, George Bush apige mbizi mara mbili kuvikwepa viatu vyake namba 10 alivyomrushia wakati akiongea na waandishi wa habari, ametoka jela jana huku akilalamika kuwa aliteswa sana alipokuwa jela.

Zaid amesema kuwa mkong'oto aliokuwa akipewa jela ulipelekea meno yake mawili yang'oke.

Zaid amesema kuwa maafisa wa jela walikuwa wakimtesa kwa kumpa adhabu mbali mbali kama vile kumpiga shoti za umeme, kumchapa kwa kutumia nyaya za umeme na mabomba ya chuma na adhabu zingine mbali mbali za kumtesa.

"Hivi sasa nipo huru lakini nchi yangu haipo huru, mimi sio shujaa lakini nina uwezo wa kuelezea maoni yangu" alisema Zaid na kuongeza "Najihisi kunyanyasika ninapoiona nchi yangu ikitaabika, Baghdad ikichomwa moto na ndugu zangu wakiuliwa" alisema Zaid muda mfupi baada ya kutoka jela.

Zaid alilakiwa na mamia ya ndugu na marafiki zake ambao walimuandalia sherehe kubwa nyumbani kwake na kumchinjia kondoo kusherehekea kurudi kwake nyumbani.

Akiongea kwenye studio za mwajiri wake wa zamani, Zaid alimtaka waziri mkuu wa Iraq, Nouri al-Maliki amuombe radhi kwa adhabu alizopewa na pia alisema atawataja maafisa wa serikali na jeshi waliokuwa wakimtesa jela.

Maisha ya Zaid yamebadilika tangia alipotoka jela kwani bosi wake amemnunulia nyumba mpya kwa ujasiri wake aliouonyesha pamoja na kuifanya televisheni yao iwe maarufu duniani.

Zaid ameahidiwa na wafanyabiashara wa kiarabu magari ya kifahari pamoja na pesa huku wanawake wengi wa Baghdad na ukanda wa Gaza wametangaza kuwania kuolewa naye.

Wakati huo huo taarifa iliyotolewa na familia ya Zaid imesema kuwa Zaid ameondoka jana jioni nchini Iraq kwenda Syria kwa ndege binafsi ambako atakaa kidogo kabla ya kuelekea nchini Ugiriki kwa matibabu ya afya yake.

source.nifahamishe.com

Mtaalamu wa Mapenzi Atamba Kulala na Wanaume 1,500

Wednesday, September 16, 2009 / Posted by ishak / comments (0)

Mwanamke huyu wa nchini Uingereza anayejiita mwenyewe Mtaalamu wa mambo ya mapenzi, amefanya mapenzi na wanaume zaidi ya 1,500 walioenda kwake kutafuta ushauri wa kimapenzi.
Katika wateja wake zaidi ya 10,000 walioenda kwake kutafuta ushauri wa kimapenzi katika kipindi cha miaka 23, mwanamke huyu anayejitamba kuwa yeye ndio mtaalamu wa masuala ya kitandani, amefanya mapenzi na wanaume 1,500 kati yao.

Mare Simone mwenye umri wa miaka 54 mkazi wa kitongoji cha Chelsea, jijini London amejiajiri mwenyewe na ana ofisi yake jijini humo akitoa ushauri wa mambo ya kimapenzi kwa wanawake na wanaume.

Baada ya kuachana na mumewe, Mare aliamua kuisomea rasmi taaluma hiyo ya mapenzi na kisha kufungua ofisi yake ambapo hadi sasa ametoa somo la mapenzi kwa zaidi ya wateja 10,000 waliofika kwenye ofisi yake katika kipindi cha miaka 23.

Mare amesema kuwa hadi sasa ameishafanya mapenzi na wanaume zaidi ya 1,500 katika wateja wake ambao miongoni mwao ni waume au wapenzi wa wanawake wengine.

Mare anasema kuwa hafikirii hata kidogo kuwa anafanya kosa lolote kinyume cha sheria kutembea na waume za watu.

"Najipatia kipato changu kwa kulala na waume au wapenzi wa wanawake wengine. Lakini mimi sifanyi ukahaba kwakuwa taaluma ya mapenzi inaruhusiwa kisheria na mapenzi yanafanyika katika mazingira ya tiba" alisema Mare.

"Watu wananilipa kwa ushauri ninaowalipa na kwa kutibu matatizo yao hawanilipi kwasababu ya ngono".

"Nasaidia kuimarisha na kubadilisha maisha ya kimapenzi ya maelfu ya wanaume na hivyo nakuwa nimesaidia kuimarisha maisha ya kimapenzi ya wake zao au wapenzi wao"

"Wanawake wengine wanabeba mimba za wanawake wengine kwasababu wanataka kuwasaidia wanawake wasio na uwezo wa kupata mimba. Hali hiyo ni sawa na mimi kwani nawasaidia watu kuwa na maisha mazuri ya kimapenzi".

Mare alielezea kuifurahia kazi yake na huwa na furaha zaidi wateja wake wanapoondoka kurudi majumbani mwao wakiwa na matumaini mapya kwenye maisha yao ya kimapenzi.

Mare kwa siku anatoa vipindi vitano vya masuala ya mapenzi na anasema wateja wake ni watu wa rika mbali mbali. "Wateja wangu ni watu wa rika zote, jinsia zote, maumbile tofauti na wafanyakazi wa vitengo tofauti tofauti".

"Wanaume mara nyingi hunifuata kwa sababu ya matatizo ya kutosimama vyema kwa uume na kufika kileleni mapema kabla ya wapenzi wao wakati wengine huambiwa waje wanione na wake zao kwakuwa hawawaridhishi kitandani".

"Kabla hawajaniona huwa wote wanapimwa magonjwa ya zinaa na lazima watumie kondomu iwapo nitalala nao" alisema Mare.

"Kwa wanawake mara nyingi hunifuata wakiwa na matatizo ya kutofika kileleni au wanapoona wapenzi wao hawajui jinsi ya kuwaridhisha kitandani".

"Huwa nawafundisha jinsi ya kujipa raha wao wenyewe na kuipenda miili yao" alimalizia Mare.

source.nifahmishe.com

Bibi wa Miaka 107 Anatafuta Mume wa 23

Tuesday, September 15, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Bibi mwenye umri wa miaka 107 wa nchini Malaysia ambaye alishaolewa na kuachika mara 21 amesema yuko tayari kuolewa na mwanaume mwingine kwa mara ya 23 kwasababu anahofia kuwa mume wake wa 22 anayeishi naye hivi sasa anaweza kumkimbia na kutafuta mwanamke mwingine mwenye umri mdogo.
Baada ya kuolewa na wanaume 21 na kuachika, bibi mwenye umri wa miaka 107 wa nchini Malaysia amesema kuwa anahofia kukimbiwa na mume wake wa 22 anayeishi naye hivi sasa ambaye miezi miwili iliyopita alikamatwa akitumia madawa ya kulevya.

Bibi Wook Kundor alipata umaarufu duniani baada ya kuolewa kwa mara ya 22 na mwanaume ambaye amemzidi jumla ya miaka 70.

Hivi sasa bibi Wook hana imani kabisa na mumewe Muhammad Noor Che Musa mwenye umri wa miaka 37 ambaye hivi sasa yuko kwenye kituo cha kurekebisha tabia akipatiwa matibabu ya kuacha utumiaji wa madawa ya kulevya.

Bibi Wook ameishaanza kusaka mume wa 23 kwani anahofia Muhammad akishatoka kwenye kituo hicho na kuacha tabia yake ya kutumia madawa ya kulevya anaweza kumkimbia na kutafuta mwanamke mwingine wa rika lake.

"Katika siku za hivi karibuni kuna hofu imeniingia" alisema bibi Wook huku akiwa ameshikilia picha yake.

"Najua kwamba mimi ni mwanamke niliyezeeka. Sina umbile la kuvutia tena na kwa umri wangu siwezi kumvutia mwanaume yoyote"

"Nia yangu ya kuolewa tena ni kuepuka upweke na si kwa sababu yoyote ile" alisema Wook na kuongeza kuwa anajihisi mpweke sana wakati huu ambao mumewe yuko mbali.

Bibi Wook alisema kuwa angependa kusherehekea sikukuu ya Eid el-Fitr wiki ijayo akiwa pamoja na mumewe.

Wook alisema kuwa ana mpango wa kumtembelea Muhammad kwenye kituo chake cha kurekebisha tabia jijini Kuala Lampur iwapo majirani zake watampeleka huko kwa gari.

Muhhamad alifunga ndoa na bibi Wook miaka mitatu iliyopita akisema kuwa urafiki wa karibu na heshima uligeuka kuwa mapenzi ya kweli.

source nifahamishe.com