MWanamke afia gesti kuitatanishi, Kimara

Thursday, December 17, 2009 / Posted by ishak / comments (0)

MWANAMKE ambaye hakuweza kufahamika jina wala makazi yake anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25 na 30, amekutwa amekufa katika nyumba ya kulala wageni iitwayo Marangu huko Kimara jijini Dar es salaam.
Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye, amesema tukio hilo limetokea jana majira ya saa 5 asubuhi, huko maeneo ya Kimara Mwisho.


Alisema maiti ya mwnwamke huyo ilikutwa ikiwa imelala kitandani huku mdomoni ikiwa inatoka mapovu na haikuweza kufahamika mara moja chanzo cha kifo hicho.


Alisema kuwa, mwanamke huyo alifika katika gesti hiyo Desemba 13, majira ya saa 4 asubuhi na alipanga katika nyumba hiyo akiwa na kijana mmoja aliyejitambulisha kwa jina la James Joshua, mkazi wa jijini Dar es Salaam.


Katika maelezo yaliyopatikana katika nyumba hiyo ilidaiwa kuwa, kwa mara ya mwisho mwanamume aliyeuingia gesti na dada huyo aliaga kwa mhudumu mmoja alyekuwa zamukuwa anakwenda kutafuta chakula aina ya chipsi na hakurejea tena.


Amesema baada ya wahudumu kutaka kuingia katika chumba hicho kwa nia ya kufanya usafi, ndipo walipobaini dada huyo kuwa aklikuwa ameshakufa.

Maiti imehifadhiwa Hospitali ya Mwananyamala na polisi wanaendelea kumsaka kijana huyo kwa udi na uvumba.


source.nifahmishe.com

Aua Watu Wawili Ili Ahukumiwe Kunyongwa

Thursday, December 17, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanaume mmoja wa nchini China ambaye alikuwa na nia ya kujiua baada ya kushindwa kupata kazi kwa muda mrefu, amewaua watu wawili ili ahukumiwe kunyongwa.
Mwanaume huyo alikuwa na nia ya kujiua lakini alikuwa hana ujasiri wa kuitoa roho yake mwenyewe. Aliamua kuwaua watu wawili ili ahukumiwe adhabu ya kunyongwa.

Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 20 ambaye alitajwa kwa jina moja tu la Bin, alichukua uamuzi huo kutokana na hali ngumu ya maisha aliyokuwa nayo baada ya kushindwa kupata kazi kwa muda mrefu.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya mji wa Jiangmen katika jimbo la Guangdong, Bin aliwaua watu wawili kwa kuwanyonga ili ahukumiwe adhabu ya kifo.

"Kwa muda mrefu sina kazi, sina uwezo wa kujiua mwenyewe, nimefanya mauaji ili nihukumiwe kunyongwa", alisema Bin.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na polisi, Bin hana uhusiano wowote na wala alikuwa hawajui watu aliowaua.

source.nifahmishe.com

Mtoto wa Miaka 10 Apandishwa Kizimbani Kwa Ubakaji

Thursday, December 17, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Watoto wawili wa kiume wa nchini Uingereza wenye umri wa miaka 10 wamepandishwa kizimbani wakituhumiwa kumbaka mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 8.
Watoto hao wakisindikizwa na ndugu zao walipandishwa kizimbani katika mahakama ya Uxbridge, magharibi mwa mji wa London, wakikabiliwa na kesi ya ubakaji.

Katika tukio hilo lililotokea oktoba 27 mwaka huu, watoto hao wanatuhumiwa kushirikiana kumbaka mtoto wa kike mwenye umri wa miaka minane wakati walipokuwa wakicheza kwenye bustani ya Hayes, iliyopo magharibi mwa London.

Watoto hao kila mmoja amefunguliwa mashtaka mawili ya ubakaji.

Waliachiwa kwa dhamana wakati uchunguzi wa kesi yao ukiendelea na watapandishwa tena kizimbani tarehe 28 mwezi ujao.

Kutokana na umri wa watuhumiwa hao, vyombo vya habari vimewekewa masharti na mahakama katika kuripoti tukio hilo.

Vyanzo vya mahakama vimeelezea kushtushwa na kesi hii ya ubakaji kutokana na umri mdogo sana wa watuhumiwa.

Kwa mujibu wa sheria za Uingereza umri wa mtoto kufunguliwa mashtaka ya jinai ni miaka 10. Nchini Scotland sheria zinaruhusu kuwafunguliwa mashtaka watoto wenye umri wa miaka minane. Umri huo ndio mdogo kulinganisha na nchi zingine za barani ulaya.

source.nifahmishe.com

Mwanamke Ajifungua Mtoto Gym Akinyanyua Vyuma

Thursday, December 17, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamke aliyeiwakilisha nchi ya Chile kwenye mashindano ya Olimpiki ya kunyanyua vitu vizito, alikuwa hajui kama ana mimba, amejifungua mtoto ndani ya gym wakati akifanya mazoezi ya kunyanyua vyuma.
Elizabeth Poblete, 22, mwanamichezo aliyeiwakilisha Chile kwenye mashindano ya kunyanyua vitu vizito kwenye olimpiki mwaka jana nchini China, amejifungua mtoto ndani ya gym alipokuwa akifanya mazoezi ya kunyanyua vitu vizito.

Elizabeth alikuwa hajui kama ana mimba na alijifungua mtoto huyo kwenye gym iliyopo kwenye mji wa Sao Paulo nchini Brazili alikoweka makazi yake.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na tovuti ya habari ya Globo.com, Elizabeth alijifungua mtoto wa kiume ambaye amempa jina la Eric Jose.

Akiongelea tukio hilo kocha wake wa gym, Horacio Reis, alisema kuwa alikuwa hajui kama Elizabeth alikuwa na mimba kwani wiki iliyopita aliweza kushiriki na kushinda kwenye mashindano ya kubeba vyuma yaliyofanyika nchini Chile.

"Mashindano yalimalizika salama na alishinda", alisema kocha wake.

Kwa mahesabu ya madaktari, Elizabeth alikuwa na mimba ya miezi sita lakini kutokana na lishe na mazoezi aliyokuwa akifanya, mzunguko wake wa damu za hedhi ulikuwa hauna mpangilio maalumu hivyo kumfanya asigundue kuwa ana mimba.

Elizabeth aliiwakilisha Chile kwenye mashindano ya olimpiki yaliyofanyika Beijing, China mwaka jana.

Katika miezi ya karibuni, alikuwa kwenye mazoezi makali na lishe ya nguvu ili kuupandisha uzito wake kutoka kilo 75 hadi 85.


source.nifahamishe.
com

Ajali Yasababisha Awe na Hamu ya Mapenzi Wakati Wote

Thursday, December 17, 2009 / Posted by ishak / comments (0)


Mwanamke mmoja wa nchini Marekani maisha yake yamebadilika baada ya kupata ajali ambayo imesababisha awe na hamu ya kufanya mapenzi muda wote. Msuguano wa nguo na mwili wake husababisha awe kwenye kilele cha mapenzi bila hata kuguswa na mwanaume yoyote.
Kutokana na ajali ya gari ambayo ilisababisha madhara kwenye mishipa ya fahamu inayokatiza kwenye nyonga yake, Joleen Baughman mwenye umri wa miaka 39 amekuwa akikabiliwa na hali ambayo humtesa masaa 24 ya kila siku.

Ajali hiyo iliyotokea miaka miwili iliyopita, ilisababisha mshipa wa fahamu uliopo kwenye nyonga ambao husimamia matamanio ya kimapenzi ya binadamu uwe kama umeachiliwa kufanya kazi muda wote.

Wakati wote Joleen hutamani kufanya mapenzi bila hata kutosheka.

Kutokana na hali hiyo, kitendo cha kukaa kwenye kiti, kuinama na hata kutembea ndani ya chumba chake husababisha mambo yawe si mambo kwenye nyeti zake bila hata kuguswa na mtu yoyote sehemu hizo.

Joleen ambaye ni mama wa watoto wawili mkazi wa New Mexico, Marekani alisema "Ni hali ambayo nashindwa kujizuia, hata msuguano wa nguo nilizovaa na mwili wangu husababisha niwe kwenye hamu kubwa sana ya kufanya mapenzi".

Joleen ambaye anaishi na mumewe Brian, 39, na watoto wao wawili anakabiliwa na ugonjwa unaowapata watu wachache sana unaoitwa "Restless Genital Syndrome".

Joleen alipata ajali mwezi aprili mwaka 2007 wakati alipokuwa kwenye gari na mumewe na gari lao kugongana uso kwa uso na gari la mwanaume aliyekuwa amelewa madawa ya kulevya.

Joleen alilazwa hospitali wiki kadhaa baada ya kufanyiwa operesheni ya ubongo na uti wake wa mgongo ambao nao ulivunjika katika ajali hiyo.

Alipona taratibu na kuruhusiwa kurudi nyumbani kwake lakini baada ya miezi sita madhara ya ajali hiyo yalianza kujitokeza.

Joleen ambaye awali alikuwa sio mpenzi sana wa kufanya mapenzi, alianza kushikwa na hamu ya ajabu ya ngono muda wote.

Awali yeye na mumewe wa ndoa ya miaka 20 walifurahia hali hiyo kwa kuwa mumewe alikuwa akipenda sana kufanya tendo la ndoa.

"Brian alikuwa na furaha kwamba kwa mara ya kwanza katika ndoa yetu mimi ndio nalazimisha kufanya mapenzi muda wote", alisema Joleen.

"Ndani ya siku moja kwa mfano tungefanya mara ya kwanza, tuliporudia mara ya pili ndio kwanza hamu yangu ya kimapenzi huanza kuongezeka, tunapoenda raundi ya tatu huwa nahisi maumivu lakini nakuwa na hamu kuliko mwanzo".

Baada ya kugundua kuwa kufanya mapenzi mara nyingi hakutatibu tatizo lake, Joleen alianza kutafuta tiba ya tatizo lake.

Alikata tamaa baada ya madaktari kumwambia kuwa tatizo lake si la kisaikolojia bali linatokana na mshipa wa fahamu unaoitwa pudendal uliopo kwenye nyonga karibu na sehemu za siri.

Kutokana na ugonjwa huo kutokuwa na tiba maalumu, Joleen bado anaendelea kusumbuliwa na tatizo hilo hadi leo.

source.nifahmishe.com