Ana Mimba ya Miezi Mitano Lakini Bado Bikira

Wednesday, January 06, 2010 / Posted by ishak /


Msichana mmoja mwenye umri wa miaka 14 wa nchini Uturuki amewashangaza wazazi wake na madaktari baada ya kupimwa na kukutwa ana mimba ya miezi mitano huku ingali bado ni bikira.
Mtoto huyo mwenye umri wa miaka 14 wa mji wa Aydin nchini Uturuki, alipelekwa hospitali baada ya tumbo lake kuzidi kuwa kubwa huku akilalamika kuwa na maumivu ya tumbo.

Baada ya vipimo vya madaktari ndipo hali ya kushangaza ilipojulikana kuwa msichana huyo ambaye bado ni bikira ana mimba ya miezi mitano.

"Alilalamika kusumbuliwa na maumivu ya tumbo huku tumbo lake likizidi kuwa kubwa ndipo tulipomleta hospitali", alisema mama wa mtoto huyo.

Wakati wazazi wa mtoto aliyetajwa kwa kifupi cha majina yake kama E.T wakiwa kwenye butwaa, daktari aliyemfanyia vipimo vya ujauzito mtoto huyo alitoa taarifa kwa uongozi wa hospitali ambao uliwapa taarifa polisi.

Katika mahojiano na polisi baba wa mtoto huyo aliyetajwa kama S.T alisema kuwa alifanya mapenzi na mkewe katika siku ambazo inasemekana mtoto wake alipata ujauzito.

"Baada ya kumaliza kufanya mapenzi na mama yake, nilijifuta mbegu za kiume kwa kutumia taulo ambalo nililiacha bafuni, inawezekana alilitumia taulo hilo kujifutia kwenye sehemu zake za siri", alisema baba wa mtoto huyo.

Baba huyo alisisitiza kuwa hakuna uwezekano hata kidogo wa mtoto wake kupata ujauzito kwa kufanya mapenzi na mwanaume nje ya nyumba yao kwakuwa mtoto wake bado ni bikira na ubikira wake umethibitishwa na madaktari.

Mtoto E.T anapatiwa matibabu ya kisaikolojia kwenye hospitali kuu ya mji huo.

source; nifahamishe

0 comments:

Post a Comment