Bei ya samaki wa Magufuli sasa ni mguu wako

Sunday, January 17, 2010 / Posted by ishak /


WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda ameitaka Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi kuhakikisha kuwa hadi kesho ugawaji wa samaki waliovuliwa kwa njia haramu katika fukwe za bahari eneo la Tanzania uwe umekamilika

Pinda alisema ikiwezekana samaki hao wagawiwe kwa mtu yeyote atakayehitaji ili kumaliza zoezi la ugawaji na kupisha shughuli nyingine za kimaendeleo

Pinda alitoa agizo hilo jana alipotembelea kiwanda cha kuhifadhia samaki hao cha Bahari Foods Ltd kilichopo Mwenge jijini Dar es salaam

Hata hivyo hadi jana tani kati ya za samaki waliohifadhiwa katika kiwanda hicho zilishapangwa kutolewe kwa taasisi mbalimbali

Katika msako uliofanywa kwa ushirikiano baina ya Tanzania na nchi zilizo ukanda huu wa Bahari ya Hindi mwaka jana jumla ya tani za samaki zilikutwa kwenye meli ya Tawaliq ya Vietnam iliyokutwa ikifanya uvuvi haramu

Pinda alisema samaki hao wamehifadhiwa katika eneo hilo kwa muda mrefu, hivyo kuwataka watendaji wanaohusika kuwagawa hata kurudia mara ya tatu kwa taasisi zilizokwisha chukua na ikiwezekana apewe yeyote

"Natoa siku mbili leo jana na kesho leo wote waliokuwa wameomba samaki hao wajitokeze kuchukua na wakisuasua kujitokeza hadi Jumatatu ikifika apewe yeyote ili waishe na tuachane na kazi hiyo" alisema Waziri Pinda.

Katika ugawaji huo pia wapo samaki aina ya vibua ambao walikuwa wakitumika kama chambo ya kuvua samaki aina ya Tuna na mchele ambavyo vyote vimedaiwa kugawiwa kwa taasisi zinazolea watoto yatima Waziri Mkuu alisisitiza kuwa endapo sekta za mifugo uvuvi na kilimo zitapuuzwa wimbo wa umaskini nchini hautaisha.

"Tukipuuza sekta hizo tutaendelea kuimba umaskini hadi mwisho kwani maeneo mengi tunang¡¦ang¡¦ania mipango ni mibovu hakuna mawazo ya maendeleo kila mahali kumejaa urasimu hali ambayo haitatutoa sehemu moja kwenda kwingine

Hivyo inabidi tujipange ili kujikwamua kupitia sekta hizo"¡¦ alisema Pinda.

Katika hatua nyingine Waziri Pinda alisema serikali italipa deni la zaidi ya Sh milioni inazodaiwa na kiwanda hicho kutokana na kuhifadhi samaki hao baada Mkurugenzi wa Kiwanda hicho Harko Bhagat kulalamikia kutokulipwa fedha licha ya Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi kulipa zaidi ya bilioni kama fedha za awali.

Awali Mkurugenzi wa kiwanda hicho, Bhagat aliilalamikia serikali kuwa inachelewesha kulipa kiasi hicho cha fedha.

Alisema kitendo hicho kinakwamisha biashara zao za uhifadhi wa samaki kutoka katika maeneo mengine wakiwemo wa kutoka ziwa Victoria.

"Inatupa wakati mgumu kibiashara lakini kwa kuwa ni serikali tumelazimika kutofuatilia hata mkataba wetu ambao ulitutaka kutokuruhusu kugawa samaki hao hadi kulipwa kwanza kwa gharama za uhifadhi ndipo tutoe, lakini tumetoa kwa kujali nchi na uzalendo hivyo ni vyema taratibu zikifanywa ili kiasi kilichobaki kikalipwa"alisema Bhagat.

Akizungumza katika ziara hiyo Waziri wa Mifugo na UvuviÆ’z Dk John Magufuli alisema fedha za kulipa uhifadhi huo ni suala mtambuka ambalo limehusisha wizara na taasisi mbalimbali likiwemo jeshi la polisi.

Nyingine kuwa ni Wizara ya Ardhi mahakama hadi ugawaji hivyo, fedha hizo wasiachiwe wizara yake pekee kuzilipa badala yake,zilipwe na wizara ya fedha kwa kuwa ndiyo yenye dhamana ya fedha nchini.

"Suala hilo sikupenda kulizungumzia muda mrefu kwa kuwa mtambuka ambalo hata hivyo nimeshawasiliana na wizara husika ili ziweze kutekeleza malipo, lakini wizara ya fedha ndiyo inayotakiwa kulishughulikia suala la ulipaji wa fedha hizo na hata bilioni tulizotoa kwa ajili ya gharama za awali tunapaswa kurudishiwa kwa kuwa suala hili ni la serikali na si Wizara yangu peke yake" alisema Dk Magufuli akimweleza waziri mkuu/

Magufuli alisisitiza kuwa baada ya kumaliza kuwagawa samaki haoÆ’z oparesheni nyingine itafanyika ili kukamata meli nyingine zinazoendelea na uharamia huo.


source mwananchi

0 comments:

Post a Comment