Haiti Yakumbwa na Tetemeko la Ardhi, Maelfu Wazikwa Hai

Friday, January 15, 2010 / Posted by ishak /


Tetemeko kubwa la ardhi lenye ukubwa wa 7.0 limeikumba haiti masaa machache yaliyopita na kupelekea maelfu ya watu kufunikwa na vifusi wakiwa hai.
Operesheni kubwa inaendelea kuwaokoa maelfu ya watu waliozikwa hai na vifusi vya majumba kufuatia tetemeko kubwa la ardhi lililotokea nchini Haiti ambalo halijawahi kutokea katika visiwa vya Caribbean.

Tetemeko hilo la ardhi lenye ukubwa wa 7.0 lilibomoa hospitali na majumba katika mji mkuu wa Haiti wa Port-au-Prince na kusababisha maafa makubwa huku kila mtu aliyesalimika akihaha kumuokoa ndugu yake au ndugu zake waliofunikwa na vifusi.

Mamia ya watu wapo chini ya vifusi wakipiga kelele za kuomba msaada.

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo lililotokea masaa machache yaliyopita alielezea jinsi alivyoiona miili ya watu ikiwa imezagaa katika mji huo ambao mawasiliano ya simu yamekatika.

Shuhuda huyo alisema kuwa maelfu ya watu wakiwa aidha wamefariki au majeruhi, walionekana mitaani ambapo barabara hazipitiki kutokana na vifusi vya majumba.

Matrekta yalionekana mitaani yakisaidia kufukua vifusi vya majumba mbali mbali yakiwemo makazi ya wanadiplomasia na wafanyakazi wa umoja wa mataifa.

Rais wa Marekani, Barack Obama ameelezea kusikitishwa kwake na maafa hayo na amesema kuwa Marekani iko tayari kutoa msaada.

"Maombi yangu na sala zangu ziwaendee wahanga wa tetemeko la ardhi, tunalifuatilia suala hili na tupo tayari kuwasaidia wananchi wa Haiti", alisema rais Obama.

ource.nifahamishe

0 comments:

Post a Comment