KALI YA MWAKA - Mtangazaji wa Italia Amfedhehesha David Beckham

Thursday, January 21, 2010 / Posted by ishak /


Mtangazaji mwanamke wa televisheni moja ya nchini Italia alimuacha nyota wa soka wa Uingereza David Beckham akiuma meno kwa hasira na fedheha baada ya mtangazaji huyo kuyakamata makende yake akiwa na nia ya kujua ukubwa wake.
Huku akipiga kelele kwa kitaliano "E piccolo, Beckham" ("Beckham kumbe ni Mdogo") mtangazaji huyo alizolewa msobe msobe na walinzi wa David Beckham baada ya kuyakamata makende yake.

Mtangazaji huyo wa televisheni moja ya nchini Italia aliyejulikana kama Elena Di Cioccio alikuwa na nia ya kujua ukweli kama mali za siri za David Beckham ni kubwa kama zinavyoonekana kwenye tangazo la chupi za Armani ambalo David Beckham alishiriki.

"Nilitaka kujua ukubwa wa makende yake", alisema Elena.

Beckham alikuwa akiongea na waandishi wa habari nje ya hoteli moja mjini Milan wakati tukio hilo lilipotokea na kumwacha Beckham akiwa hajui la kufanya akibaki anamwangalia mtangazaji huyo kabla ya walinzi wake kumuondosha.

Mtangazaji huyo alipanga tukio hilo mapema na kuongozana na timu yake ya wapiga picha hadi kwenye eneo ambalo David Beckham alikuwa akiongea na waandishi wa habari.

Huku akiwa amevaa gloves za njano, mtangazaji huyo alijipenyeza na kumsogelea kwa karibu Beckham kabla ya kuzikamata nyeti zake na kuanza kupiga kelele za "Beckham kumbe mdogo".

Beckham alishiriki kwenye matangazo ya nguo za ndani za mwanamitindo maarufu duniani Giorgio Armani. Katika picha za tangazo hilo Beckham anaonekana akiwa ameshehena mzigo kwenye sehemu zake nyeti ambao mkewe Victoria Beckham aliubatiza jina la "Golden Balls".

Hivi karibuni Cristiano Ronaldo alichukua nafasi ya Beckham katika matangazo hayo ya viwalo vya ndani vya Armani.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment