Mama Afanya Mapenzi Mara 200 na Mtoto wa Miaka 12

Wednesday, January 20, 2010 / Posted by ishak /


Mama mmoja nchini Uingereza alifanya mapenzi mara 200 na mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 12 na alikuwa akiweka alama kwenye daftari lake kila alipomaliza kufanya naye mapenzi.
Angela Sullivan mwenye umri wa miaka 36 anakabiliwa na kifungo cha miaka mingi sana jela kwa kufanya mapenzi takribani mara 200 na mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 12 .

Angela alikuwa akiweka alama ya nyota katika daftari lake kila anapomaliza kufanya mapenzi na mtoto huyo.

Katika kipindi cha miezi 10 cha uhusiano wa Angela na mtoto huyo, daftari lake lilikutwa likiwa na alama za nyota 191 kuonyesha siku walizofanya mapenzi.

Taarifa zaidi zilisema kwamba Angela alimnunulia zawadi ya viatu mtoto huyo baada ya kufanya naye mapenzi kwa mara ya 100.

Mahakama iliambiwa kuwa Angela alianza uhusiano na mtoto huyo kwa kumlewesha pombe na kisha kuzichezea sehemu zake za siri.

Hatimaye walianza uhusiano wa kimapenzi ambao ulidumu kwa miezi 10 hadi uhusiano wao ulipogundulika kufuatia uvumi kwenye shule ya mtoto huyo kuwa Angela amepata ujauzito.

Wapelelezi waligundua pia kuwa mtoto huyo ambaye hakutajwa jina lake kwasababu za kisheria, alikuwa akijigamba kwa rafiki zake kwenye internet kuhusiana na uhusiano wake wa kimapenzi na Angela.

Mahakama iliambiwa kuwa Angela alikuwa akifanya mapenzi na mtoto huyo kwenye nyumba yake katika mji wa Middlesbrough na kabla ya kuwasili kwa mtoto huyo alikuwa akimpeleka kwa bibi yake mtoto wake pekee wa kiume aliyekuwa akiishi naye.

Alipotiwa mbaroni, Angela alikanusha kufanya mapenzi na mtoto huyo lakini alishindwa kuelezea vizuri alama katika daftari lake ambazo ziliambatana na maneno kama vile "Angela anampenda ..[jina la mtoto huyo]..".

Alipofikishwa mahakamani jana, Angela alikiri makosa yake ya kufanya mapenzi na mtoto na alifunguliwa mashtaka 10, kosa moja kwa kila mwezi mmoja wa uhusiano wake na mtoto wake.

Kesi yake imeahirishwa hadi mwezi ujao huku Angela akirudishwa rumande wakati uchunguzi ukiendelea.

Angela huenda akatupwa jela maisha ili kunusuru maisha yake kutokana na hasira za wananchi.

Madirisha ya vioo vya nyumba yake yalivunjwa kwa mawe tangia siku alipotiwa mbaroni.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment