Vurugu zatanda chakula cha Mengi

Wednesday, January 20, 2010 / Posted by ishak /

KUNDI la watu ambao hawakuhitajika kuwa katika chakula cha mchana kilichoandaliwa na Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi kwa ajili ya kuwapa chakula cha mchana walemavu wa aina zote nchini walivamia katika ukumbi na kufanya fujo n
Watu hao ambao hawakuwa na chembe ya hata ulemavu walivamia katika ukumbi wa Diamond Jubilee katika sherehe hizo za 16 za kila mwaka ambapo Mengi alikuwa akiwakutanisha walemavu na kuwapa chakula cha mchana kwa pamoja.

Watu hao waliodiriki kufanya fujo mbele ya mgeni rasmi Waziri Mkuu Pinda na kuvamia majofu yaliyokuwa na vinyaji na kugombania vinyaji hivyo kwa fujo hali iliyofanya kuharibu mandhari ya ukumbi mzima katika sherehe hizo.

Katika hali ya kushangaza watu hao ambao walisemekana ji wahuni wa mitaani waliingia kwenye ukumbi huo na kuvamia majokofu hayo na kufanya fujo hizo na hatimaye baadhi ya walemavu nao kuingia katika fujo hizo na wao wakionekana kugombania vinywaji hivyo.

Vinywaji vilivyokuwa vikigombaniwa ni pamoja na bia za kopo aina zote pamoja na soda za kop ambazo ziliandaliwa kwa ajili ya shuhuli hiyo.

Kufuatia hali hiyo askari polisi walikuwa wachache ukumbini hapo na kuzidiwa na kundi huilo la wahuni na hatimaye vinywaji hivyo kutkidhi haja ya wageni waliohudhuria sherehe hizo naw ahuni hao kujazad viroba walivyokuja navyo na kuondoka na vinywaji hivyo.

Risala, hotuba walizokuwa wakitoa wageni rasmi ukumbini humo zilikuwa zikisikika kwa tabu kutokana na makelele yaliyokuwa ukumbini humo hali iliyofanya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kushanga hali hiyo mbele ya macho yake.

Hali hiyo ilisababisha hadi Pinda wakati anataka kuondoka nje ya ukumbi huo kuondoka kwa shida kutokana na kukosekana kwa njia iliyotokana na vurugu hizo za kugombea vinywaji.
Watu walisukumana na kupigana kwenye maeneo yaliyopangwa kwa ajili ya kutoa huduma ya vinywaji.

Baadhi ya wafanyakazi wa IPP waliiambia NIFAHAMISHE kuwa "wanashangazwa na vurugu hizo kwa sababu vinywaji vilikuwepo vya kutosha kwa ajili ya watu hao, lakini wakaongeza kuwa watu ambao hawakukusudiwa kwa hafla hiyo, ndio waliovamia na kufanya vurugu hizo kwa kuwa hali kama hiyo haijawahi kutokea katika miaka yote ambayo Mengi huandaa chakula cha mchana.

Katika hafla hiyo iliyokutanisha watu wenye ulemavu tofauti, na walemavu wapatao 4000 walikutanishwa katika ukumbi huo klwa ajili ya chakula hicho ambapo sherehe hizo hufanyika wka mwaka mara moja.

Katika chakula hicho viongozi mabalimbali walihuduria akiwemo na askofu wa KKKT Askofu Malasusa, Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkuu wa Majeshi nchini.

Pia wabunge wawakilishi wa walemavu bungeni walihudhuria sherehe hizo.


Sherehe hizo zilifanyika Jumapili mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Diamondi Jubilee.

Pia wasanii mbalimbali walijumuika katika sherehe hizo kutumuiza walemavu akiwemo, TID, MARLOW,DIAMOND, DULLY SYKES, WANAUME TMK, na MWASITI

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment