Amuua Mpenzi Wake Baada ya Kuambiwa Hayawezi Majambozi

Tuesday, February 16, 2010 / Posted by ishak /

Mwanaume mmoja nchini Uingereza amefikishwa mahakamani kwa kumuua mpenzi wake aliyemkebehi kuwa ana uume mdogo sana hivyo hawezi kumtosheleza hamu zake za kimapenzi.
Peter Ling, 50, aliiambia mahakama kuwa alishindwa kuzitawala hasira zake baada ya kipenzi chake Linda Casey kumwambia kuwa hana kiungo cha siri kikubwa cha kuweza kumtosheleza hamu zake za kimapenzi, limeripoti gazeti la Daily Mail la Uingereza.

Ling, aliandaa sehemu ya starehe jijini London kwaajili ya kukutana na Linda akiwa na nia ya kumuuliza kama Linda ana mwanaume mwingine pembeni.

Baada ya kukutana na baadae kufanya naye mapenzi, Ling alimgeukia Linda na kuanza kumhoji kuhusiana na emails alizozituma zinazohusiana na tovuti za kutafuta wachumba na pia kama ana mwanaume mwingine pembeni.

Wakati wa mabishano yaliyozuka wakati huo, Linda aliongelea masuala ya viungo vya siri vya Ling akimuambia kuwa uume wake ni mdogo sana kuweza kumtosheleza.

"Nilikuwa ni kama bomu lililokuwa likisubiria kulipuka wakati wowote, alipotoa maoni hayo moja kwa moja yalizama kwenye akili zangu", Ling aliiambia mahakama.

"Siku zote nimekuwa nikiushuku ukubwa wa uume wangu", aliongeza Ling.

Baada ya Linda kutoa maoni hayo, Ling alianza kumshushia kipigo Linda mpaka alipofariki.

Ling anaitaka mahakama iamue kesi hiyo kama mauaji bila kukusudia badala ya kesi ya mauaji ya kukusudia aliyofunguliwa.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment