Atoweka nyumbani baada ya kupata ‘0’ matokeo ya kidato cha nne

Friday, February 12, 2010 / Posted by ishak /

MSICHANA Joyce Aloyce [18] mkazi wa Shekilango jijini Dar es Salam, ametoweka nyumbani kwao baada ya kupata majibu yake ya kidato cha nne yaliyoonyehsa amefeli mitihani hiyo na kupata divisheni 0.

Msichana huyo ametoweka nyumbani kwao na hajulikani alipo na mama yake kupata na wasiwasi na kujua mwanae huyo yuko wapi na hajui pa kumpata wapi.

Mama huyo aliyekutana na Mwandishi wa habari hii katika kutuo cha Urafiki cha jijini akija kuripoti tukio hilo kwa msaada zaidi.

Mama huyo aliiambia nifahamishe kuwa binti yake huyo hamuoni takribani wiki sasa na kusema toka matokeo hao yatoke na kujigundua kuwa alipata ziro basi hakurudi nyumbani hapo kwa kuhofia kufukuzwa nyumbani kwao hapo kwa kuwa mzazi ake wa kumu alishamwambia awali kabla ya matokeo.

Alidai walipoona kinywa kinazidi walijaribu kupita kwa ndugu zao wa karibu ambao wangehisi labda angekuwa huko lakini bila mafanikio hawakuweza kumkuta wka ndugu yoyote na kutojua yuko wapi kwa sasa.

Alidai kutokana na hali hiyo familia hiyo wameanza kuogopa na wamekuja kuripoti kituoni hapo na taratibu zingine zinaendela za kwenda kumsaka na mikoni huenda atakuwa amekwena kujichimbia huko kwa kujhofia aibu na kupigwa na baba yake.

Mama huyo alidai binti huyo ni mtoto wake wa pili na kuonyesha huzni kubwa kwa kuwa motto wa kike katika familia hiyo hiyo aliuwa jni yeye tu kati ya watoto wannne alio nao.

“Mimi naweza kumsamehe hata akirudi nyumbani ila mume wangu sijui kama ataweza kumsamehe, wanaume wanakuwa wakali hata watoto wanawaogopa sasa mwanangu ametoweka nyumbani kwa kumuogopa baba yake” huku akionekana kutokwa na machozi kwa mkasa huo uliomkuta


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment