Meseji yazua utata kwa wanandoa

Monday, February 08, 2010 / Posted by ishak /

MWANAMKE mmoja [32] [jina kapuni] mkazi wa Ukonga Mombasa jijini Dar es Salaam,anamlazimisha mume wake ampe talaka kinguvu kwa kushindwa kuvumilia baada ya kukuta meseji ya kimapenzi kwenye simu ya mume wake.

MWanamke huyo alimtaka mume wake huyo ampe talaka kwa kukuta meseji ambayo inamfanya akose raha kwenye nyumba yake hiyo na kudai kuwa anaweza akamfanya kitu kibaya mume wake huyo na kuomba bora apewe talaka kwa kuepusha matatizo.

MWanamke huyo alikuta ujumbe wa simu kutoka kwa hawara wa mumeme huyo, uliomfanya akose raha na baada ya kumuuliza mume wake huyo alimjibu kuwa huyo dada wakikuwa wakitaniana mara kwa mara na kumsihi mkewe huyo kuwa haikuwa kweli.

Ujumbe alioufuma dada huyo kutoka kwenye simu hiyo ulisema kuwa “ nimekumisi sana mpenzi wangu, penzi lako la jana lilikuwa zuri sana sitaweza kulisahau, naomba tuoanane kesho jioni” ulisema ujumbe huo

Baada ya kukuta meseji hiyo dada huyo alihamisha ujumbe huo kwenye simu yake na kuhamisha kwenye line nyingine ya simu ya ziada na kisha kumuuliza mumewe huyo kama alikuwa na uhusiano na mwanamke mwingine.

ALidai kuwa, mumewe huyo alikana kuwa na mahusiano na mwanamke mwingine bila kutambua kuwa mke wake huyo aliangalia ujumbe uliohifandiwa katika simu yake hiyo.

Alidai alimuuliza mara ya pili na kumwambia kuwa alikuwa anahitaji talaka yake kwa kuwa alibaini ana mahusiano na mwanamke mwingine alipoendelea kubisha alichukua simu na kumuonyesha ujumbe huo na baba huyo kukosa jibu kwa muda huo na kumwambia kuwa huyo dada walikuwa wakitaniana mara kwa mara.


Baba huyo alianza kumsihi mke wake asiwe na jazba kwa kuwa haikuwa kweli ila ni utani ambao walikuwa wakitaniana na huyo dada mara kwa mara.

Maelezo yake hayo hakuweza kuyaelewa na kumuamuru ampe talaka ili kila mtu aweze kuishi kwa amani kwa kuwa alishamuudhi kupita kiasi.

HAdi nifahamishe inaandika habari hii ilipofanya mawasiliano na dada huyo alikuwa hajapata talaka hiyo na ameondoka nyumbani kwake hapo na kwenda kupumzika kwa rafiki yake ili aweze kupata talaka hiyo.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment