Siku ya Wapendanao Patakuwa Hapatoshi Kwenye Mgahawa Huu

Monday, February 08, 2010 / Posted by ishak /


Katika kusherekea siku ya wapendanao duniani, Valentine's Day, mgahawa mmoja wa nchini Kanada unawaalika wateja wake kufanya mapenzi kwenye vyoo vya mgahawa huo.
Mgahawa wa Mildred's Temple Kitchen wa mjini Toronto nchini Kanada umeibuka na staili ya ajabu ya kuwavutia watu kwenye mgahawa huo kusherehekea siku ya wapendanao (februari 14).

Mgahawa huo unawaalika wateja kufanya mapenzi kwenye vyoo vya mgahawa huo.

Meneja wa mgahawa huo, Rory Gallagher, alisema kuwa katika kusherekea siku ya wapendanao, kuanzia februari 12 hadi februari 15 watu wataruhusiwa kufanya mapenzi kwenye vyoo vya mgahawa huo.

Gallagher aliendelea kusema kuwa ili kufanya mambo yote yaende sawa, mgahawa huo umeandaa wafanyakazi ambao watakuwa na jukumu la kuviweka safi vyoo hivyo wakati wote.

Akiongea na gazeti la The Toronto Star, mmoja wa wamiliki wa mgahawa huo, Donna Dooher, alisema "Watu wamekuwa wakifanya mapenzi kwa siri kwenye vyoo vyetu, tunataka siku ya wapendanao iwe ya kipekee".

Hata hivyo mmiliki huyo alisema kuwa wateja watatakiwa kuja na kondomu zao wenyewe.

Katika hali ya kushangaza zaidi, Ofisi ya masuala ya afya ya jamii ya Toronto imeuruhusu mgahawa huo kuendelea na mipango yake hiyo huku ikitoa taarifa kuwa mgahawa huo hauvunji sheria yoyote kwakuwa vitendo vya kujamiiana havitafanyika jikoni, vitafanyika kwenye vyoo ambavyo vitawekwa safi wakati wote.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment