Watano wafariki kwa kufunikwa na kifusi –Dodoma

Tuesday, February 16, 2010 / Posted by ishak /

WATU watano wamefariki dunia papo hapo jana, baada ya kufukiwa na kifusi wakati wakiwa wanachimba kokoto huko katika kijiji cha Ntyuka, mkoani Dodoma
Waliofariki katika tukio hilo ni wanawake watatu na watoto wawili ambao walikuwa na mama zao eneo la tukio.

Wanawake hao ni Monica Chizumi na mwanawe Porina Chizumi mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu, Mwajuma Mnubi na mtoto wake, Jonas Mnubi wa mwaka mmoja na miezi 8 na Mbeleje Ndingomo

Mbali na waliokufa dunia watu wengine wawili ambao ni Beatrice Chizumi na Noel Lazaro alijeruhiwa na walikimbizwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma baada ya kunusurika katika tukio hilo.

Tukio hilo la kusikitisha lililotokea jana majira ya saa 7 mchana kijijini humo.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment