Achaniwa nguo na wapiga debe

Friday, March 05, 2010 / Posted by ishak /

MSICHANA mmoja jina lake halikuweza kupatikana maramoja alijikuta yupo kwenye wakati mgumu baada ya kuchaniwa nguo yake aliyovaa na wahuni na kumuacha na aibu kedekede na akiwa hana la kufanya kwa wakati huo.
Tukio hilo la aibu lilitokea jana majira ya saa 2 usiku, maeneo ya Magomeni Kagera wakati msichana huyo akiwa kituoni hapo akisubiri usafiri.

Wahuni hao walianza kumshambulia kwea maneno dada huyo na msichana huyo kuwajibu jeuri na hivyo wahuni hao waliamua kumchania nguo yake ya isiyo na heshima aliyoivaa.

Msichana huyo alivaa nguo fupi kupita kiasi, alivaa blauzi tu na kuigeuza gauni hivyo kupelekea maungo yake ya mwili kuonekana ambapo wahuni hao waliamua kumfanyia uhuni kumchania ng uo hiyo ili atembee kama alivyozaliwa kabisa.

Wahuni hao walimshika dada huyo na kumchania gauni hilo na kupiga kelele na hakuna hata msamaria mwema mmoja aliyeweza kumsaidia wka wakati huo kwa kuwa hakuna mtu aliyependezwa na uvaaaji wake huo.

Wahuni hao ambao walikuwa zaidi ya wawili walishirikiana kwa pamoja kumshikisha adabu dada huyo na kumuacha akilia kituoni hapo na nguo yake kuichana.

“Tumeanza na wewe leo, na wengine watafuata tunataka mpate adabu si mteembee uchi tu” walisikika wakaka hao

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment