Akamatwa akiwa katika zoezi la kuiba mtoto

Monday, March 22, 2010 / Posted by ishak /

MWANAMKE mmoja amekamatwa akiwa anazungukazunguka mazingira katika nyumba moja huku akimemendea kuondoka na mtoto aliyelazwa barazani mwa nyumba hiyo .

Tukio hilo lilitokea jana huko maeneo ya Buguruni kwa Mnyamani, majira ya jioni, huku mama huyo alionekana kwa muda mrefu akizunguka nyumba hiyo bila ya wakazi hao kutambua dhumuni la mama huyo.

Ilidaiwa kuwa mama huyo alikuwa akipita njia hiyo mara kwa mara na wenyeji wa nyumba hiyo wakidhani kuwa alikuwa amepotea ramani ya alipotaka kuelekea bila kutambua dhumuni lake.

Kumbe mama huyo lengo na madhumuni yake alikuwa anasubiri watu waishio humo wazubae na kumuacha mtoto huyo nay eye amuibe na aondoke nae.

Bila kutambua mama wa mtoto huyo baada ya mtoto huyo kulala alichukua mto na kumlaza mtoto huyo barazani hapo na kuingia ndani na watu wengine waliendelea na shughuli zao bila kutambua kuwa mtoto huyo alikuwa anaviziwa.

Hivyo dakika chache mama huyo alpoach kisogo na kuingiga ndani mama huyo mwizi alisogea maeneo hayo na kutaka kumchukua huyo mtoto ghafla mama wa mtoto huyo alitoka na kumkuta mama huyo akwia barazani hapo na kumshangaa.

Mama huyo alitaka kukimbia kabla hajakimbia mama wa mtoto huyo alimdaka na kumuhoji alikuwa anahitaji nini kwa muda huo ili aweze kumsaidia na mama huyo kukosa jibu la uhakika na kumjibu kuwa alipita hapo na kuona mdudu alikuw anataka kumsogelea mtoto huyo na ndipo alisogea kumuondoa mdudu huyo.

Majibu hayo yalimtia mashaka mama wa mtoto huyo na kuita wenzake waliopanga katika nyumba hiyo na kumuhoji mama huyo bila majibu.

Ndipo mmoja wao alipopataw azo na kuwaambia wenzake huenda alikuwa anataka kumuiba mtoto huyo na wakashtuka na wakampeleka kituo cha polisi ili akaoe maelezo.

Kabla hajafika kituoni mama huyo aliwaomba wanawake wenzake hao wamsamehe kwa kuwa alikuwa na lengo l kuiba mtoto huyo na aliomb wasimpeleke kituo cha polisi.

NIFAHAMISHE ilibahatika kumuona watu wa mtaa huo walivyojazana mahali hapo na wakimpeleka kituoni mama huyo.

Mama wa mtoto huyo alipozungumza na nifahamishe alidai kuwa “ mimi na wenzangu tulikuwa tunamuona mama huyu akipita njia hii mara kwa mara na tulikuwa hatuelewi alikuwa na dhumuni gain, kumbe inaonekana anapitaga hapa na kumuona mtoto analazwa hapa nje na leo alikwu anamsalandia

“Ujue mimi kutokana na sasa hivi kuwa na joto kali sana ndani naamuaga kumlaza mwanangu hapa nje ili aweze kulala vizuri kwa kuwa kunakuwa na upepo hapa barazani'

Mama huyo alifikishwa kituo cha polisi ili aweze kusalimika huku baadhi ya watu wakiokuwa na jazba wangeweza kumjeruhi, hadi nifahamishe inondoka kituoni haikuweza kuongea na mkuu yoyote kituoni hapo na itafatilia kujua hatma ya mama huyo kituoni hapo leo.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment