Amfumania Mkewe na Wanaume Wawili, Awaua Wote

Sunday, March 14, 2010 / Posted by ishak /


Mwanaume mmoja wa nchini Marekani ambaye aliingia nyumbani kwa mpenzi wake na kumkuta mpenzi wake akifanya mapenzi na wanaume wawili kwa mpigo, anashikiliwa na polisi kwa kumuua mpenzi wake na wanaume hao wawili aliowafumania nao.
Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 50 mkazi wa Brooklyn, New York aliingia kwenye nyumba ya mpenzi wake na bila kutarajia alimkuta mpenzi wake akifanya mapenzi na wanaume wawili kwa wakati mmoja.

Mwanaume huyo alimuachia ujumbe wa sauti rafiki yake kuwa amemuua mpenzi wake mwenye umri wa miaka 51 baada ya kumfumania akifanya mapenzi na wanaume wawili kwa mpigo.

Polisi walipewa ujumbe huo wa sauti na kuwahi kwenye nyumba ya mwanamke huyo na kumkuta mwanaume huyo akiizunguka maiti ya mpenzi wake.

Mwanaume huyo alikiri mbele ya polisi kuwa alishikwa na hasira sana baada ya kumfumania mpenzi wake akiliwa mtungo na wanaume wawili, alimuua mpenzi wake na wanaume hao wawili na kisha kuikatakata vipande vipande miili ya wanaume hao na kwenda kuitupa kwenye vichaka.

Jirani mmoja wa mwanaume huyo alisema kuwa mwanaume huyo hakuonekana kutetereka wala kujutia mauaji aliyoyafanya, aliinamisha kichwa chake chini wakati alipokuwa akipandishwa kwenye karandinga la polisi, liliripoti gazeti la New York Post.

Polisi wanaendelea kumshikilia mwanaume huyo na uchunguzi wa kesi yake unaendelea.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment