Matiti ya Bandia Yaokoa Maisha Yake

Wednesday, March 03, 2010 / Posted by ishak /


Mwanamke wa nchini Marekani ambaye alitandikwa risasi ya kifua baada ya kujifanya amefariki, alinusurika maisha yake kutokana na matiti ya bandia aliyoyapandikiza kwa operesheni miaka kadhaa iliyopita.
Lydia Carranza alikuwa kazini kwake kwenye zahanati ya meno mjini California wakati mume wa mfanyakazi mwenzake alipovamia kwenye zahanati hiyo.

Mwanaume huyo alikuwa amebeba bunduki na alifika kwenye zahanati hiyo akiwa na lengo moja tu la kumuua mkewe ambaye alikuwa akidai talaka.

Kaka wa mke wa mwanaume huyo ambaye naye anafanya kazi kwenye zahanati hiyo aliingilia kati akitaka kusuluhisha mambo lakini alitandikwa risasi ya tumbo na mwanaume huyo.

Baada ya hapo mwanaume huyo alimgeukia mkewe na kuanza kumpiga risasi kadhaa mpaka alipohakikisha amemuua.

Ndipo sasa zamu ilipomuangukia Coranza na wafanyakazi wenzake. Coranza alitandikwa risasi kwenye mkono wake wa kulia, alipojifanya amefariki mwanaume huyo alimsogelea na kumtandika risasi nyingine ya kifua.

Coranza ambaye ni mama wa watoto watatu alinusurika maisha yake kutokana na matiti ya bandia ya silicone aliyojipandikiza miaka kadhaa iliyopita kuhimili kishindo kikubwa cha risasi hiyo.

Miaka michache iliyopita Coranza alifanya operesheni ya kuongeza ukubwa wa matiti yake kutoka saizi B hadi saizi D.

"Ana bahati sana, risasi ilibakia milimita chache sana kuufikia moyo wake na ogani zake muhimu, kama angekuwa hajafanya operesheni ya kuongeza matiti, tusingekuwa tunaongea hivi sasa", alisema Dr. Ashkan Ghavami wa zahanati hiyo alipokuwa akiongea na gazeti la Los Angeles Times.

Jaime Paredes, mwanaume aliyefanya mashambulizi hayo ya risasi alikamatwa na anasubiria kupandishwa kizimbani akikabiliwa na mashtaka mbali mbali yakiwemo mashtaka ya mauaji ya mkewe.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment