MAZISHI YA KIFAHARI NDANI YA TANZANIA

Wednesday, March 03, 2010 / Posted by ishak /


MAZISHI YA ASKARI WA BWANA YESU KRISTO MAJOR NASSON JOHN KITUTA AMBAYE NDIYE MMOJA WA WAANZIRISHI WA JESHI LA WAKOVU HAPA TANZANIA (THE SALVATION ARMY).
MAZISHI YA ASKARI WA BWANA YESU KRISTO MAJOR NASSON JOHN KITUTA AMBAYE NDIYE MMOJA WA WAANZIRISHI WA JESHI LA WAKOVU HAPA TANZANIA (THE SALVATION ARMY)
Azikwa kifahari kama viongozi wa serikali ya Nyerere.

Mmoja wa wanzilishi wa shirika la kikristo la Salvation Army hapa nchini Major Nasson Kititu mwenye umri wa miaka 83 alizaliwa mwaka 1926 june 6 na amefariki dunia tarehe 26 februari katika hospitali ya Mikocheni, na kuzikwa katika shamba lake lililopo Kongowe Dar es Salaam,

Alipata Kujiunga na Jeshi la wokovu mwaka1948 akiwa chunya alifunga ndoa na mke wake 'Maria Kititu' mwaka 1950 katika wilaya ya chunya mkoani mbeya,mwaka wa 1951 aliitikia wito wa kumtumiki mungu kama mchungaji akamua kwenda katika chuo cha uchungaji cha jeshi la wokovu Nairobi.

Baada yakumaliza mafunzo ya uchungaji alianza kazi kama Luteni wa Jeshi la wokovu kanisa la Igunga 1952 hadi 1955

Katika mazishi yake kulikuwa na mvua nyingi ilinyesha kuashiria kuwa alikuwa mtumishi wa mungu mamia ya waumini wakiwemo majirani ndugu jamaa walihudhulia katika mazishi ambayo hakiki yalikuwa kama ya mtu mmoja wa kifahari kabisa na yenye heshima kuu kama mtumishi wa mungu yakiwa yameongozwa na COLONEL HEZEKIEL MAVUNDLA ambaye ni kiongozi wa Mkuu wa makanisa ya Salvation Army Tanzania. ambaye ni raia wa South Africa

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment