Mpemba kortini kwa kulawiti watoto wanne kwa mpigo

Thursday, March 18, 2010 / Posted by ishak /

SELEMANI RASHIDI mkazi wa mtaa wa Utete Ilala jijini Dar es Salaam, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashitaka ya kulawili watoto wanne wenye umri wa miaka kumi .
Mshitakiwa huyo mwenye asili ya kipemba, alifikishwa mahakamani hapo mwishoni mwa wiki iliyopita akikabiliwa na mashitaka hayo.

Alifikishwa Mbele ya Hakimu Mkazi Genevitus Dudu, na upande wa Mashitaka ulikuwa ukisimamiwa naWakili wa Serikali, Abubakar Mrisho wote wa maakma hiyo.

Ilidaiwa kuwa, mshitakiwa alilawiti watoto hao wanne huku akijua ni kosa kisheria. Na amekwenda kinyume cha kifungu cha 154(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai kama ya mwaka 2002.

Ilidaiwa kuwa, Februari 15 mwaka huu, majira ya saa nane mchana, huko Mtaa wa Kilwa na Utete, Ilala nyumba namba 1, kwa mshitakiwa aliwalawiti watoto wanne wenye umri kati ya miaka minane na kumi.

Mshitakiwa huyo alikana shitaka hilo na wakili wa kujitegemea Mabere Marando aliiomba mahakama impatie mteja wake dhamana kwa kuwa mashitaka yanayomkabili yanadhaminika kisheria.

Hata hivyo, Hakimu Mkazi Dudu alisema hakuwa kwenye nafasi nzuri ya kutoa masharti ya dhamana, hivyo akaamuru mshitakiwa apelekwe rumande hadi Machi 17 mwaka huu, siku ambayo atatoa masharti ya dhamana.

Hivyo mshitakiwa alirudishwa rumande na atarudishwa tena kesho kwa kutajwa na atakwua nje wka dhamdana endapo hakimu atatoa masharti ya dhamana.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment