Njaa Mbaya Sana, Wanakijiji Zimbabwe Wamla Tembo

Friday, March 12, 2010 / Posted by ishak /


Kweli njaa si mchezo, wanakijiji wa kijiji kimoja nchini Zimbabwe ambacho kimekumbwa na janga la njaa na umaskini, wanakijiji wake walitumia dakika 105 tu kumchuna ngozi tembo aliyekutwa amefariki na kisha kujisevia nyama zake na mwishoe hakuna hata
Ndani ya lisaa limoja na dakika 45 tembo aliyekutwa msituni amefariki, alichunwa ngozi na kisha wanakijiji walianza kujisevia nyama zake na kubakisha mifupa tu ikiwa imezagaa kwenye eneo ambalo tembo huyo alifariki.

Mifupa ya tembo huyo nayo ilipitiwa na wanakijiji wengine siku iliyofuatia na hivyo kufanya eneo alilofariki tembo huyo liwe jeupee bila dalili ya kufariki kwa mnyama yoyote yule.

Tukio hilo lilitokea katika kijiji kimoja nchini Zimbabwe ambapo inasemekana mifupa ya tembo hutumika kutengenezea sabuni.

Tukio la wananchi kujisevia nyama ya mzoga wa tembo huyo halikufanyika kwa utulivu na hali ya vurugu na ngumi zilizuka wakati wanakijiji wakipigania kupata chochote cha kuganga njaa.

Picha za tukio hilo zinaonyesha jinsi hali ngumu ya maisha na njaa inavyowafanya watu wale mpaka mizoga.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment