Obama Atakiwa Aache Kuvuta Sigara

Wednesday, March 03, 2010 / Posted by ishak /


Rais Barack Obama wa Marekani ametakiwa aache kuvuta sigara na daktari wake.
Rais Obama ametakiwa na daktari wake aache kabisa kuvuta sigara kwaajili ya afya yake mwenyewe.

Obama aliambiwa hivyo baada ya vipimo vya kwanza vya afya yake tangia alipochaguliwa kuwa rais wa Marekani kuonyesha kuwa ana afya njema sana na yupo fiti kulitumikia taifa lake.

Daktari binafsi wa Obama, Jeffery Kuhlman alisema kuwa vipimo vya afya ya Obama vimeonyesha kuwa Obama atakuwa mwenye afya njema kipindi chote cha urais wake.

Dr. Kuhlman alimshauri Obama aendelee na jitihada zake za kujizuia kuvuta sigara ili aiche kabisa tabia ya kuvuta sigara.

Rais Obama mwenye umri wa miaka 48, amekuwa akijitahidi kujizuia kuvuta sigara mbele za watu na amesema kuwa siku hizi huwa havuti sigara mbele ya familia yake.

Enzi zake kabla ya urais, Obama alikuwa mvutaji mkubwa sana wa sigara na kuna wakati Michelle Obama alinukuliwa na jarida moja la Marekani akielezea kukerwa na uvutaji sigara wa Obama.

Rais Obama alimuahidi mkewe kuwa akishinda urais ataacha kabisa kuvuta sigara lakini alikiri kuwa amekuwa akivuta sigara siku moja moja tangia alipoingia ndani ya ikulu ya Marekani.

Mwaka jana rais Obama alisema kuwa amefanikiwa kujizuia kuvuta sigara kwa asilimia 95.
source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment