ontena za betri bandia zakamatwa

Monday, March 22, 2010 / Posted by ishak /

SHEHENA ya kontena 20 za betri aina ya Tiger Head kutoka China zimekamatwa kutokana na kukosa ubora na viwango vya matumizi ya bidhaa hiyo.
Kontena hizo zimekamatwa katika operesheni ya Shirika la Viwango nchini (TBS) kayitka kukagua bnidhaa ziingiazo nchini ambazo hazina viwango vya matumizi.


Mkurugenzi Mkuu wa TBS Charles Ekerege alisema shehena waliyokamata ya betri hizo ilifika nchini Januari mwaka huu, lakini walipozikagua wakagundua kuwa hazina ubora uliowekwa na shirika hilo.

Alisema Betri hizo zinaingizwa nchini na wafanyabiashara wakubwa na wakati mwingine imedaiwa kuwa wanaziingiza kwa njia ya panya.

Alisema betri hizo huingizwa nchini na huuzwa kwa bei ya rejereja shilingi 350 na zinazotengenezwa hapa nchi huuzwa kwa shuilingi 45o kila moja, na watanzania wengi hukimbilia betri hizo kutokana na unafuuu wa bei.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment