Polisi Mwanamke Mwenye Pepo la Ngono Asimamishwa Kazi

Sunday, March 07, 2010 / Posted by ishak /


Afisa mmoja wa polisi mwanamke wa nchini Australia amesimamishwa kazi kutokana na usumbufu anaowapa maafisa wa polisi wa kiume kwa kuwabembeleza afanye nao mapenzi.
Afisa wa polisi Jessica Parfrey mwenye umri wa miaka 19, amesimamishwa kazi kutokana na usumbufu anaowapa maafisa wenzake wa kiume kwa kuwataka afanye nao mapenzi.

Ndani ya siku chache za kuanza kazi kama afisa wa polisi wa mjini Sydney nchini Australia, Jessica alimtongoza bosi wake akimwambia kuwa "Kila mtu anajua kuwa unatakiwa uwe na uhusiano wa kimapenzi na mfanyakazi mwenzako".

Mwezi mmoja baada ya kuona bosi wake hana dalili zozote za kukubali, Jessica alimfuata na kumwambia "Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 19, unaonaje tukifanya mapenzi tu, hivi wewe una matatizo gani?"

Mahakama ya mambo ya kazi iliambiwa pia kuwa Jessica alifanya mapenzi na afisa mwingine wa polisi kwenye choo cha baa.

Jessica hakuishia hapo, alimsumbua afisa mwingine mwanaume wa polisi kwa kumpigia simu mara 12 na kumtumia meseji sita kabla ya kumuahidi kumsaidia afisa huyo kwenye mtihani wake wa mambo ya polisi. Jessica alimwambia afisa huyo kuwa kwa kila swali moja atakalopata basi yeye atasaula nguo yake moja. Afisa huyo alikataa dili hilo.

Awali Jessica alisimamishwa kazi mwishoni mwa mwaka 2007 lakini alikata rufaa akisema kuwa matukio ya yeye kuwataka maafisa wenzake yalitokea wakati wakiwa baa nje ya muda wa kazi.

Mahakama ya kazi ya mjini Sydney ilitoa uamuzi wake juzi na kuitupilia mbali rufaa ya Jessica.

Mahakama hiyo iliunga mkono hukumu iliyotolewa awali ya kumfukuza kazi Jessica kwa kukiuka maadili ya kazi na kuwasumbua maafisa wenzake.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment