Mamia ya Wakristo Wajipigilia Misumari Kwenye Misalaba

Sunday, April 04, 2010 / Posted by ishak /


Mamia ya waumini wa Kikristo nchini Philippines walitumia dakika kadhaa wakiwa kwenye maumivu makali wakati walipoadhimisha siku ya kusulubiwa kwa yesu kwa kupigiliwa misumari ya sentimeta tano kwenye miguu na mikono yao.
Bila ya kutumia ganzi misumari ya sentimeta tano ilipigiliwa kwenye mikono na miguu ya waumini wa Kikristo katika kukumbushia kusulubiwa kwa mkombozi wa wakristo, Yesu Kristo.

Mwanamke aliyejitambulisha kwa jina la Mary-Jane Mamangun alidai kuwa hakusikia maumivu yoyote wakati misumari ya sentimeta tano ilipokuwa ikipigiliwa kwenye miguu na mikono yake.

Lakini sura yake wakati alipotundikwa msalabani ilionyesha wazi maumivu makali aliyokuwa akiyapata na alilazimika kuwahishwa kwenye hema la matibabu ambapo alipatiwa dawa za kupunguza maumivu.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment