Amaliza Shule Akiwa na Umri wa Miaka 94

Tuesday, May 18, 2010 / Posted by ishak /


Elimu haina mwisho wala umri, hivyo ndivyo alivyothibitisha bibi wa Marekani mwenye umri wa miaka 94 mwenye wajukuu na vitukuu 41 ambaye mwishoni mwa wiki alisherehekea kumaliza elimu ya shahada ya kwanza na kuwa kikongwe wa pili duniani kumaliza elimu ya juu.
Bibi Hazel Soares, mwenye umri wa miaka 94 wa Oakland, Marekani alikuwa miongoni mwa wanafunzi 500 waliotunukiwa shahada mbalimbali za chuo kikuu.

"Imenichukua muda mrefu sana kumaliza digrii kwakuwa nilikuwa bize sana kwenye maisha yangu",alisema Soares ambaye sasa anamiliki digrii ya Art history.

Soares, ana watoto sita na wajukuu na vitukuu wapatao 40, anashika nafasi ya pili duniani kwa kumaliza digrii akiwa na umri mkubwa sana.

Nola Ochs wa Kansas ndiye anayeshikilia rekodi ya kumaliza digrii akiwa na umri mkubwa kuliko watu wote duniani. Alitunukiwa digrii miaka mitatu iliyopita baada ya kumaliza masomo yake kwenye chuo kikuu cha Fort Hays State University wakati huo akiwa na umri wa miaka 95.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment