Amuua Mkewe Na Kisha Kuila Maiti Yake

Monday, May 17, 2010 / Posted by ishak /


Mwanaume mmoja wa nchini Marekani amehukumiwa kwenda jela miaka 15 baada ya kumuua mkewe kwa kumchoma choma na kisu mara 250 na kisha kula nyama za mapafu yake kabla ya kunywa damu yake mbele ya mtoto wake wa miaka minne.
Mohammad Solaiman alihukumiwa kwenda jela kati ya miaka 15 na kifungo cha maisha kwa kumuua kikatili mkewe Shahida Sultanna ndani ya nyumba yao mjini New York katika tukio lililotokea mwaka 2007.

Binti yao mwenye umri wa miaka minne alikuwa chumba cha pili wakati baba yake alipokuwa akimuua mama yake na alishuhudia kitendo cha baba yake akinywa damu ya mama yake.

"Alichukua maini na mapafu yake na kuyatafuna", alisema dada wa marehemu na kuongeza "Alikunywa damu yake, binti yake ameniambia".

Wakili wa Solaiman, John Scarpa alikanusha madai ya Solaiman kumgeuza asusa mkewe ingawa alikubali kumuua mkewe.

Wakili huyo aliendelea kusema kuwa Solaiman alikuwa akipigwa na kunyanywaswa sana na mkewe na hiyo ndio sababu iliyompelekea kufanya mauaji.

Akitoa hukumu ya kesi hiyo, jaji Richard Buchter alisema kuwa faili la mshtakiwa halikusema chochote kama alikuwa akinyanywaswa na mkewe.

"Tunachojua ni kwamba, mshtakiwa alimchoma na kisu mkewe usoni, shingoni, tumboni, mgomgoni na kwenye maeneo yake ya siri", jaji Buchter alisema.

"Kuthibitisha kitendo chake cha kikatili alimuonyesha binti yake wa miaka minne mabaki ya mwili wa mama yake", aliongeza jaji Buchter.

Solaiman alihukumiwa kwenda jela kati ya kifungo cha miaka 15 na kifungo cha maisha baada ya kukiri kufanya mauaji hayo.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment