Arekodi Video Za Binti Yake Akifanya Mapenzi

Thursday, May 20, 2010 / Posted by ishak /


Mama wa nchini Marekani ambaye alirekodi VIDEO za binti yake mwenye umri wa miaka 16 akiingiliwa kinguvu na mpenzi wake ametupwa jela miaka 58 jela.
Bobbie Jo Geveshausen mwenye umri wa miaka 43 alipenda kurekodi video wakati mpenzi wake Edward D. Shockey alipokuwa akifanya mapenzi na binti yake mwenye umri wa miaka 16 na wakati mwingine alijiunga nao.

Kutokana na tabia yake hiyo, Bobbie atatupwa jela miaka 58 kwa kushiriki kwenye kitendo cha kuingiliwa kinguvu kwa binti yake huku yeye mwenyewe akiwa ndio mchukuaji wa video.

"Ni vigumu kuamini kuwa mama mzazi anafurahia binti yake kubakwa huku akirekodi video", alisema mwendesha mashtaka wa kitongoji cha Platte, Eric Zahnd kabla ya jaji kutoa hukumu jana.

Video za kuingiliwa kinguvu kwa binti yake Bobbie ziligundulika baada ya Edward kumpa kimakosa mpenzi wa binti huyo DVD ambazo zilitakiwa ziwe ni za muziki.

Badala yake DVD hizo zilimuonyesha Edward akimuingilia kinguvu binti huyo ambaye katika baadhi ya matukio ya DVD hizo alionekana wazi kuwa ni mjamzito.

Katika DVD hizo mama yake alionekana pia akishiriki katika baadhi ya matukio ya kuingiliwa kwa binti yake.

DVD hizo zilipelekwa polisi ambapo Edward na Bobbie walitiwa mbaroni muda mfupi baadae.

Wakati Edward alihukumiwa kwenda jela miaka 25, Bobbie alihukumiwa kwenda jela miaka 58 baada ya kukiri makosa matano ya kumuingiza binti yake mwenye umri mdogo kwenye masuala ya ngono na makosa mawili ya kulawitiwa kwa binti yake .

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment