Kila Anayemiliki Namba ya Simu Hii Hufariki

Wednesday, May 26, 2010 / Posted by ishak /


Shirika la simu la Mobitel la nchini Bulgaria limeamua kuifuta mojawapo ya namba zake za simu baada ya kugundulika kuwa kila mtu anayeimiliki namba hiyo hufariki baada ya muda mfupi.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Bulgaria, wamiliki wa namba ya simu hii 0888 888 888 hufariki ndani ya kipindi cha muda mfupi.

Shirika la simu la Mobitel la nchini Bulgaria ambalo linaimiliki namba hiyo limeamua kuifutilia mbali namba hiyo baada ya taarifa ya vifo vya wenye kuimiliki namba hiyo.

Mtu wa kwanza kufariki alikuwa ni bosi wa kampuni hiyo kubwa ya simu nchini Bulgaria, Vladimir Grashnov, ambaye alifariki mwaka 2001 kutokana na ugonjwa wa kansa.

Namba hiyo ya simu alipewa mtu mwingine aliyejulikana kwa jina la Konstantin Dimitrov ambaye naye alifariki miaka miwili baadae baada ya kupigwa risasi nchini Uholanzi.

Inasemekana kwamba mabosi wa kundi la Mafia wa Urusi ndio waliopanga mauaji yake baada ya kumuonea wivu kwa jinsi alivyokuwa akisafirisha kwa wingi madawa ya kulevya.

Mfanyabiashara Konstantin Dishliev alipewa namba hiyo baada ya Konstantin kufariki lakini naye alifariki miaka miwili baadae baada ya kupigwa risasi nje ya mgahawa wa vyakula vya kihindi mjini Sofia nchini humo.

Mfanyabiashara huyo inasemekana alikuwa akisafirisha madawa ya kulevya toka nchi za kusini mwa America kuziingiza Bulgaria. Aliuliwa baada ya polisi kuugundua mzigo wake wa madawa ya kulevya ukiwa njiani kuingizwa Bulgaria.

Mobitel wameamua kuifuta namba hiyo baada ya polisi kukumbana nayo mara kadhaa katika upelelezi wao wa baadhi ya vifo vya watu vilivyohusishwa na madawa ya kulevya.

Namba hiyo hivi sasa haipatikani tena na mtu anapojaribu kuipiga hupewa ujumbe "Namba unayopiga haipo kwenye mtandao wetu".

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment