Kila Nyumba Tanzania Kuwa na Maji ya Uhakika Ifikapo Mwaka 2013

Wednesday, May 26, 2010 / Posted by ishak /


RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa kero ya maji nchini inatarajiwa kuisha kabisa ifikapo mwaka 2013.
Hayo aliyasema jana katika ukumbi wa Karimjee katika majumuisho ya ziara yake ya siku moja jijini Dar es Salaam.

Alisema upo mradi mkubwa unaotarajiwa kuanza mapema mwaka huu wa kuvuna maji yaliyoko ardhini katika eneo la Kimbiji ambao ukikamilika mwaka 2013 vyanzo vyote vitakuwa na uwezo wa kutoa maji lita milioni 710 kwa siku ikiwa ni pamoja na kukamilika kwa upanuzi wa vyanzo vya maji vya Ruvu Chini na Ruvu Juu.

Alisema kwa sasa mahitaji ya maji katika Jiji la Dar es Salaam ni lita milioni 450 lakini zinazopatikana ni lita milioni 300 kutoka vyanzo mbalimbali ikiwemo Ruvu chini na Juu, Mtoni na visima.

Rais Kikwete aliwaagiza watendaji wa halmashauri zote wakishirikiana na Mamlaka ya Majisafi na Majitaka (DAWASA) na Shirika la Majisafi na Majitaka (DAWASCO) na Wizara ya Maji na Umwagiliaji kuondoa kero ya maji katika kipindi cha mpito kwa kuchimba visima vingi virefu na kumaliza kero hiyo ya maji inayowasumbua wananchi.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment