Panya Ndani ya Ikulu ya Obama

Friday, May 21, 2010 / Posted by ishak /


Hotuba ya Rais Barack Obama wa Marekani iliingiliwa na kitu asichokitegemea baada ya panya kukatiza mbele yake wakati akitoa hotuba ndani ya ikulu ya Marekani.
Rais Barack Obama alikuwa akitoa hotuba kwenye bustani maarufu ya Rose Garden iliyopo mbele ya ikulu wakati panya alipojitokeza na kukatiza mbele yake toka upande mmoja kwenye upande mwingine.

Wapiga picha waliokuwepo eneo la tukio hawakupitwa na panya huyo na walifanikiwa kuchukua taswira wakati kiumbe hicho kilipokuwa kikipita mbele ya mkuu wa taifa kubwa duniani.

Haijajulikana kama rais Obama alimuona panya huyo au la kwani alielendelea na hotuba yake bila kutetereka.

Taarifa zinasema kwamba panya huyo alionekana pia akipiga misele kabla ya Obama hajaanza kutoa hotuba yake.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment