Uingereza imepata waziri mkuu mpya David Cameron toka chama cha Conservative baada ya chama cha Labour kupigwa mwereka kwenye uchaguzi mkuu. Kiongozi

Wednesday, May 12, 2010 / Posted by ishak /


Hizi ni picha za kusikitisha za mwanaume mwenye umri wa miaka 25 wa nchini Uingereza ambaye alipewa kipigo na kisha kumwagiwa tindikali baada ya kutuhumiwa anamchukua mke wa mtu.
Awais Akram alijeruhiwa vibaya baada ya kumwagiwa tindikali na hata baada ya matibabu makubwa mwili wake umebaki na majeraha yanayotisha kuanzia kichwani mpaka miguuni.

Sura ya Akram imeharibika vibaya sana wakati nywele zale zinamea kwenye sehemu ya mbele tu ya kichwa chake ambayo ilinusurika na tindikali.

Majeraha zaidi ya tindikali yapo pia sehemu mbalimbali za mwili wake kama vile kifuani, tumboni, mgongoni, miguuni na mikononi.

Yote haya yaliyomkumba Akram yalisababishwa na mwanamke mwenye umri wa miaka 24 aliyefahamiana naye kwenye FaceBook aliyejulikana kwa jina la Sadia Khatoon.

Kaka yake Sadia aliyeitwa Vakas aligundua uhusiano wao baada ya kuwaona pamoja mitaani na alipogundua wanawasiliana kwa kutumia mtandao wa FaceBook alithibitisha kuwa dada yake anaisaliti ndoa yake.

Mume wa Sadia, Shakeel Abassi na yeye alipogundua uhusiano wa Akram na mkewe kwenye FaceBook, alikula njama na kaka yake Sadia wamteketeze Akram kwa kuingilia ndoa za watu.

Sadia alilazimishwa na kaka yake aliyeshirikiana na mumewe amlaghai Akram afike kwenye eneo ambalo wao walipanga kufanya shambulizi lao.

Akram naye bila kujua hili wala lile alijitosa kwenye eneo la tukio akijua anaenda kukutana na Sadia.

Alipofika kwenye eneo la tukio, Akram alijikuta akipewa kipigo cha nguvu kabla ya kumwagiwa tindikali iliyomuunguza sehemu kubwa ya mwili wake.

Akram alinusurika maisha yake lakini hadi leo bado anaendelea kupatiwa matibabu.

Sadia na mumewe walifanikiwa kutoroka Uingereza na kukimbilia kwao Pakistan ambako inasemekana wanaendelea kujificha huko.

Kaka yake Sadia, Vakas alikamatwa na jana ndio ilikuwa hukumu yake kwenye mahakama ya Old Bailey jijini London.

Vakas alipatikana na hatia ya kufanya jaribio la kuua mtu na alihukumiwa kwenda jela miaka 30.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment