Wanafunzi Wanyonyana Sehemu za Siri Darasani Huku Mwalimu Akichekelea

Sunday, May 16, 2010 / Posted by ishak /


Mwalimu mmoja wa nchini Marekani anafanyiwa uchunguzi baada ya kuwaachia wanafunzi wake wanyonyane sehemu za siri darasani huku wanafunzi wengine wakichukua video za tukio hilo na kupiga picha.
Televisheni ya KTLA ya Marekani imeripoti kuwa tukio hilo limetokea kwenye shule ya Haydock Intermediate School iliyopo Oxnard, California ambapo mwanafunzi wa kike na wa kiume walinyonyana sehemu za siri darasani mbele ya wanafunzi wenzao waliojaa darasani kwaajili ya kuangalia filamu iliyoandaliwa na mwalimu huyo.

Mwanafunzi wa kiume wa darasa la nane na mwanafunzi wa kike wa darasa la saba ndio waliohusika katika tukio hilo ambalo limewakasirisha wazazi wengi nchini Marekani.

Wanafunzi walichukua video za tukio hilo kwa kutumia simu zao huku wengine wakipiga picha ambapo mwalimu wao alipuuza na hakuchukua hatua yoyote ile kuzuia kitendo hicho kiovu darasani.

Mwalimu huyo amepewa likizo yenye malipo wakati uchunguzi wa tukio hilo ukiendelea.

Wanafunzi waliofanya kitendo hicho hawajachukuliwa hatua yoyote na wanahudhuria shuleni kama kawaida.

Sylvia Ramirez, mmoja wa wazazi ambaye anafanya kazi katika mgahawa wa shule hiyo alisema kuwa ameiona video ya ngono ya wanafunzi hao.

"Inasikitisha sana kuona hawalitilii uzito suala hili, shoo ya ngono inafanyika darasani, inasikitisha sana", alisema Ramirez.

Polisi wanalifanyia uchunguzi tukio hilo baada ya kupewa taarifa.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment