Wanawake Watakaovaa Vimini Kuvalishwa Sketi Ndefu

Wednesday, May 26, 2010 / Posted by ishak /

Serikali ya Indonesia imeandaa sketi ndefu 20,000 kwaajili ya kuwavalisha kinguvu wanawake watakaokamatwa barabarani wakiwa wamevaa vimini au nguo zinazobana.
Kuanzia leo polisi wa kiislamu wa Indonesia wanaingia mitaani kuwasaka wanawake wanaovaa nguo fupi au zinazobana zinazoonyesha maumbile yao, wanawake watakaokamatwa mitaani wakiwa wamevaa hivyo watalazimishwa wavae hapo hapo sketi ndefu zilizotolewa bure na serikali.

Hatua hiyo imefuatia sheria ya kupiga marufuku nguo fupi za wanawake ambayo inaanza kufanya kazi leo katika mojawapo ya majimbo ya nchi hiyo yenye waislamu wengi kuliko nchi zote duniani.

Sheria hiyo imepitishwa katika jimbo la Aceh lililopo kaskazini mwa kisiwa cha Sumatra nchini Indonesia. Vimini, jeans na nguo za kubana ni miongoni mwa nguo za wanawake zilizopigwa marufuku.

Mkuu wa jimbo hilo Ramli Mansur alisema kwamba wanawake watakaosimamishwa na polisi wa sharia, hawatatiwa mbaroni lakini watalazimishwa wavae sketi ndefu zilizotolewa na serikali.

Mansur aliongeza kwamba ataisimamia vyema sheria hiyo kwa kuhofia siku moja ataulizwa na Mungu aliutumiaje uongozi wake katika kusimamia sharia za kiislamu.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment