Achomwa Kisu Kwa Kulalamikikia Miguno ya Ngono ya Jirani

Thursday, June 24, 2010 / Posted by ishak /

Mwanaume mmoja nchini Marekani amechomwa kisu na jirani yake baada ya kulalamikia sauti kali za ngono anazozitoa anapofanya mapenzi na mpenzi wake.
Mwanaume mwenye umri wa miaka 40 aliyejulikana kwa jina la Russell Willis Shepherd Jr. amefunguliwa mashtaka ya kumshambulia jirani yake mwenye umri wa miaka 58 ambaye alikuwa akilalamika miguno ya kimahaba aliyokuwa akiitoa.

Katika tukio hilo lililotokea South Carolina nchini Marekani, jirani wa Russel alirudi nyumbani kwake na kumkuta Russel akitoa sauti kali wakati akifanya mapenzi na mpenzi wake mwenye umri wa miaka 39.

Kuepuka kelele hizo aliamua kwenda nje kuvuta sigara, aliporudi na kukuta kelele hizo zikiwa ndio zimepamba moto, aliamua kumgongea mlango Russel na kumwambia apunguze kelele za ngono anazozitoa.

Russel alikasirishwa na kitendo hicho, alichukua kisu na kuanza kumshambulia jirani yake huyo mpaka alipofanikiwa kuchoropoka na kuomba msaada toka kwa jirani.

Russel almefunguliwa mashtaka ya kufanya shambulizi la kudhuru mwili na ametupwa jela akisubiri kufikishwa mahakamani.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment