Afukua Maiti Toka Kaburini na Kufanya nayo Mapenzi

Tuesday, June 29, 2010 / Posted by ishak /


Kijana mwenye umri wa miaka 20 wa nchi ya kusini mwa Amerika ya Guyana amewashangaza watu wengi kwa kitendo chake cha kufukua maiti ya bibi wa miaka 75 na kisha kufanya nayo mapenzi.
Kijana huyo aliyetajwa kwa jina la Roopram Bacchus ambaye hufanya kazi ya kuokota taka, alipandishwa kizimbani ijumaa kujibu mashtaka yanayomkabili.

Bacchus alikiri mashtaka aliyofunguliwa ya kufanya mapenzi na maiti.

Kijana huyo alikiri kulifukua kaburi la bibi mwenye umri wa miaka 75 na kisha kufanya mapenzi na maiti yake.

Bacchus alijitetea kuwa ana matatizo ya kupenda sana pombe ambayo ndiyo iliyompelekea akafanya kitendo hicho.

Jaji aliamuru afanyiwe uchunguzi wa akili zake na alimuamuru alipe faini ya dola 200 za Kimarekani. Atatupwa jela mwaka mmoja kama akishindwa kulipa faini hiyo.

Kamanda wa polisi wa eneo hilo, Steve Merai alisema kuwa Bacchus alilifukua kaburi la bibi huyo siku moja baada ya bibi huyo kuzikwa.

"Bacchus alilivunja jeneza, aliitoa maiti toka kwenye jeneza na alifanya nayo mapenzi", alisema kamanda huyo wa polisi.

Kamanda huyo wa polisi aliongeza kuwa Bacchus na familia ya bibi huyo walikuwa ni majirani.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment