Aozeshwa Ng'ombe Aliyembaka, Azimia Wakati wa Harusi

Tuesday, June 15, 2010 / Posted by ishak /


Kijana mmoja wa nchini Indonesia ambaye alilazimishwa kumuoa ng'ombe aliyembaka, alizimia wakati wa harusi yake na ng'ombe huyo.
Kijana Ngurah Alit mwenye umri wa miaka 18 alikamatwa kwenye kijiji chake cha Yeh Embang katika kisiwa cha Bali nchini Indonesia, akiwa uchi wa mnyama akifanya mapenzi na ng'ombe.

Alit alijitetea kuwa ng'ombe huyo ndiye aliyemtongoza yeye na kumvutia kufanya naye mapenzi.

Alit alidai kuwa aliamini kuwa ng'ombe huyo alikuwa ni msichana mrembo ambaye alikuwa akimfanyia mitego mbalimbali ili afanye naye mapenzi.

Pamoja na utetezi wake, Alit alilazimishwa amuoe ng'ombe huyo na harusi ya kitamaduni iliandaliwa.

Wakati polisi wakiwaweka waandishi wa habari mbali na eneo la harusi, Alit alizimia kabla ya kukabidhiwa rasmi 'mke' wake.

Hata hivyo Alit aligeuka mjane punde baada ya harusi baada ya bi harusi wake kuzamishwa kwenye bahari kama mojawapo ya imani za kijiji hicho.

Ili kusafishika na kitendo chake, Alit aliogeshwa kwenye ufukwe wa bahari.

Mkuu wa kijiji hicho alisema baada ya harusi hiyo kuwa kijiji sasa kimesafishika baada ya tukio hilo lililoleta aibu kwenye kijiji.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment