Bakora 90 na Jela Miezi 4 Kwa Kubusiana Hadharani

Friday, June 11, 2010 / Posted by ishak /

Mahakama nchini Saudi Arabia imemhukumu mwanaume aliyembusu mwanamke hadharani kucharazwa bakora 90 na kwenda jela miezi minne.
Mahakama mjini Riyadh, Saudi Arabia imemhukumu mwanaume aliyembusu mwanamke kwenye shopping mall kwenda jela miezi minne.

Mahakama pia imeamuru mwanaume huyo acharazwe bakora 90 kwa kitendo chake hicho.

Kwa mujibu wa gazeti la kila siku la serikali la Al-Yom, polisi wa kidini wa Saudia walimtia mbaroni mwanaume huyo pamoja na wanawake wawili baada ya kuwaona wakifanya vitendo nje ya maadili mbele ya watu wengine.

Mwanaume huyo ambaye umri wake ni kwenye miaka ya 20, alionekana akiwa amekaa na mwanamke mmoja wakibusiana na kukumbatiana. Haikuelezewa mwanamke wa pili alikuwa akifanya nini wakati huo.

Majina ya wanawake hao na mwanaume huyo hayakutajwa.

Kwa mujibu wa sheria za kiislamu nchini Saudia, ni kosa mwanaume na mwanamke ambao hawana uhusiano wowote (hawajaoana) kuongozana barabarani achilia mbali kukaa pamoja na kuanza kubusiana.

Gazeti la Al-Yom liliripoti kuwa mwanaume huyo atacharazwa bakora 90 kwa mafungu matatu na pia amepigwa marufuku kuingia kwenye shopping mall yoyote nchini humo kwa miaka miwili.

Wanawake aliokamatwa nao watasomewa mashtaka yao katika mahakama nyingine.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment