Hatimaye Sio Mungu Tena..

Sunday, June 13, 2010 / Posted by ishak /


Mtoto aliyezaliwa nchini India akiwa na mikono minne na miguu minne ambaye alikuwa akiabudiwa kama mungu amepoteza uungu wake baada ya kufanyiwa operesheni kuondoa mikono na miguu iliyozidi.
Deepak Paswan, 7, alizaliwa katika sehemu za watu masikini nchini India akiwa ameungana na pacha wake kwenye tumbo. Alikuwa na miguu minne na mikono minne lakini kichwa kimoja.

Waumini wa dini ya Hindu katika kijiji chake kilichopo kwenye jimbo la Bihar walikuwa wakimtembelea nyumbani kwake wakimuabudu kama Mungu wa Kihindu anayeitwa Vishnu.

Familia yake haikufurahia jinsi mamia ya watu walivyokuwa wakienda nyumbani kwao kwaajili ya kumuabudu mtoto huyo na waliomba msaada kwa watu ili mtoto huyo afanyiwe upasuaji.

Hatimaye maombi yao yalikubaliwa mei 30 mwaka huu na hospitali moja katika mji wa Bangalore ilikubali kulipa gharama zote za kumfanyia operesheni mtoto huyo.

Baada ya operesheni ngumu ya masaa manne, madaktari walifanikiwa kuondoa viungo vilivyozidi toka kwenye mwili wa mtoto huyo.

Deepak akitambulishwa mbele ya waandishi wa habari, alionekana kufurahia hali yake mpya ambayo imempotezea sifa yake ya uungu ambayo waumini wa Hindu walimpa.

"Siku zote tulitaka afanyiwe operesheni ili atenganishwe na pacha wake aliyejiunga tumboni mwake ili kuepuka watu kumfanya mtoto wetu chombo cha ibada", alisema baba wa mtoto huyo Viresh Paswan.

"Hatimaye ndoto yangu imetimia sasa tutafanya sherehe tutakaporudi kijijini kwetu", alisema Paswan.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment