Imamu Mwanamke Anapowasalisha Wanaume

Sunday, June 13, 2010 / Posted by ishak /



Mwanamama wa Kanada Raheel Raza kama ilivyotarajiwa jana aliweka rekodi kwa kuwa mwanamke wa kwanza wa kiislamu nchini Uingereza kusalisha sala ya ijumaa. Raheel aliwaambia waumini waliokuwepo msikitini kuwa si dhambi katika uislamu mwanamke kusalisha wanaume.
Mwandishi wa habari wa Kanada ambaye pia mwanaharakati wa kupigania usawa wa kijinsia katika dini ya kiislamu, Raheel Raza jana aliweka rekodi ya kuwa imamu mwanamke wa kwanza nchini Uingereza.

"Nilikuwa mwanamke wa kwanza kuwa imamu nchini Kanada, mwanamke kusalisha wanaume si dhambi, hata mtume wetu ametoa ruhusa ingawa baadhi ya maimamu wanakubali na wengine wanaona si sahihi ni makosa", alisema Rahel.

"Mimi kabla ya kutoa uamuzi wangu nilifanya utafiti na nimegundua kuwa ni sahihi na hamna kosa lolote".

"Nimetumiwa email nyingi za vitisho vya kuuliwa ili nisirudie tena kuwa imamu, hata hivyo mimi uimamu sio kazi yangu, nimekuja hapa baada ya kuitwa na watu", alisema Rahel.

Naye kiongozi wa kituo cha waislamu cha Oxford, Dr. Taj Hargey, ambaye ndiye aliyemualika Rahel kuja kusalisha katika kituo chao, alisema kuwa wanawake kuongoza misikiti si suala la kujadili.

"Hakuna aya katika Quran inayokataza wanawake kusalisha au kuongoza misikiti, katika uislamu wanaume na wanawake ni sawa. Kama katika misikiti hakuna usawa wa jinsia basi katika jamii pia hakutakuwa na usawa", alisema.

"Huenda ikawa ni vigumu kuwa na imamu mwanamke nchini Saudi Arabia au Pakistan lakini haimanishi kuwa ni makosa kuwepo sehemu zingine", aliongeza Dr. Taj Hargey.

Dr. Taj Hargey alisema kuwa sala ya jana haikukumbana na vipingamizi vyovyote hivyo inamaanisha kuwa watu wanaanza kuelewa na kukubali taratibu taratibu.

"Inabidi turudie kufanya hivi mara nyingi ili watu wazoee", alisema Dr. Taj Hargey

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment