Watu Wafupi Wako Kwenye Hatari ya Kufa Kwa Magonjwa ya Moyo

Tuesday, June 15, 2010 / Posted by ishak /


Utafiti uliofanywa kwa miaka 50 ukiwashirikisha watu milioni 3 umeonyesha ufupi ni tatizo na watu wafupi wako kwenye hatari ya kufariki kwa magonjwa ya moyo kulinganisha na watu warefu.
Baada ya miaka 50 ya utafiti wanasayansi wamegundua kuwa ufupi wa mtu ni mojawapo ya sababu zinazochangia watu kupata magonjwa ya moyo.

Utafiti huo ulionyesha kuwa watu wafupi wako kwenye hatari ya asilimia 50 zaidi ya watu warefu kupata magonjwa ya moyo.

Kwa wastani mtu alihesabika mfupi akiwa na urefu wa sentimeta 160.5 wakati mtu alihesabika mrefu alipokuwa na urefu wa sentimeta 173.9.

Utafiti huo ulionyesha usahihi kwa jinsia zote za kike na kiume ingawa kipimo cha urefu wa mwanaume na mwanamke kilikuwa tofauti.

Wanaume wafupi walitajwa kuwa na urefu chini ya sentimeta 165.4 wakati wanaume warefu walikuwa na urefu kuanzia sentimeta 177.5.

Wanawake wafupi walihesabika kuwa na urefu chini ya sentimeta 153 wakati wanawake warefu walikuwa na urefu wa sentimeta 166.4.

Kwa kuwa watu wafupi huwa na mishipa midogo ya damu ya coronary artery, hali hiyo huchangia kuwafanya wawe kwenye nafasi kubwa ya kukumbwa na matatizo ya msukumo wa damu mwilini.

Matokeo ya utafiti huu yalitolewa kwenye jarida la European Heart Journal baada ya kuwashirikisha jumla ya watu milioni 3.

Dr Tuula Paajanen, wa chuo kikuu cha Tampere nchini Finland, aliyeongoza utafiti huo alisema kuwa kwa miaka mingi kumekuwa na mjadala mrefu kuhusiana na urefu wa mtu kuwa mojawapo ya sababu za kupata magonjwa ya moyo.

Dr Paajanen alisema kuwa matokeo ya utafiti huu yanaonyesha kuwa ufupi wa mtu ni sababu inayojitegemea ya mtu kupata magonjwa ya moyo.

Dr Paajanen alisema kuwa mbali ya unene, uzee na kiwango kikubwa cha kolestro, ufupi nao inabidi uongezwe katika sababu zinazochangia matatizo ya moyo.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment