Mama Afungwa Miaka 30 Jela Kwa Kufanya Mapenzi na Mwanae

Wednesday, July 14, 2010 / Posted by ishak /


Mwanamke wa nchini Marekani ambaye alifanya mapenzi na mwanae mwenye umri wa miaka 14 amehukumiwa kwenda jela miaka 30.
Aimee Sword, 36, atatumia miaka 30 jela kwa kufanya mapenzi na mtoto wake wa kiume wa kumzaa hotelini na nyumbani kwa rafiki yake katika jimbo la Michigan.

Sword alianza kufanya mapenzi na mwanae baada ya kuwasiliana naye kupitia Facebook mwezi mei mwaka 2008 wakati huo mwanae alikuwa na umri wa miaka 14.

Kabla ya hapo Sword hakuwa na mawasiliano na mwanae huyo ambaye alimtoa kwenye nyumba ya watoto yatima wakati mtoto wake huyo akiwa na umri wa miaka miwili.

Sword ambaye ni mama wa watoto sita, alikiri kosa moja la kufanya ngono na mtoto mwenye umri mdogo na aliwaomba msamaha watoto wake na dada yake.

"Najuta kwa yote yaliyotokea.... sielewi imekuwaje", Sword aliiambia mahakama.

Sword mbali ya kuhukumiwa kwenda jela miaka 30 amepigwa marufuku kuwasiliana na mtoto wake.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment