Mwanamke Afariki Akiangalia Video ya Ngono

Friday, July 09, 2010 / Posted by ishak /


Mwanamke wa nchini Uingereza ambaye inadaiwa alikuwa na afya njema bila matatizo yoyote ya kiafya, amefariki dunia kutokana na shambulio la moyo lililosababishwa na msisimuko alioupata wakati akiangalia filamu ya ngono.
Nicola Paginton, 30, alikutwa amefariki kwenye kitanda chake huku toy la vibrator likiwa pembeni yake na filamu ya ngono ikiendelea kuonekana kwenye laptop yake, limeripoti gazeti la The Sun la Uingereza .

Daktari aliyeifanyia uchunguzi maiti ya Nicola alisema kuwa Nicola alikuwa fiti na mwenye afya njema kabla ya kifo chake cha ghafla.

"Hakuna kitu kwenye moyo wake ambacho naweza kukitaja kama sababu ya kifo chake cha ghafla", alisema daktari huyo.

Nicola inasemekana alifariki kutokana na shambulio la moyo lililomkumba ghafla baada ya mapigo ya moyo kuongezeka kwa kasi kutokana na msisimuko wa kingono alioukuwa akiupata.

Maiti ya Nicola iligundulika nyumbani kwake baada ya baada ya polisi kwenda nyumbani kwake kufuatia taarifa kuwa hajaonekana kazini kwa siku kadhaa.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment