Wazisaliti Ndoa Zao, Wadondoka Toka Ghorofani Wakila Uroda

Thursday, July 22, 2010 / Posted by ishak /


Mwanaume na mwanamke wa nchini Ujerumani ambao walizisaliti ndoa zao na kula uroda kwa siri, walianguka toka ghorofani kupitia kwenye dirisha ambalo waliliegemea wakati wakipeana uroda.
Wapenzi hao waliozisaliti ndoa zao walijikuta wakiwa uchi pembezoni mwa barabara baada ya kudondoka toka ghorofa ya kwanza katika jengo lililopo kwenye mji wa Lubeck nchini Ujerumani.

Majirani walisema kuwa wapenzi hao walikuwa wakikutana mara kwa mara katika nyumba hiyo.

"Hatukuwaona wakati wakifanya mapenzi lakini tulizisikia sauti walizokuwa wakizitoa", alisema mmoja wa majirani.

Polisi walisema kwamba wapenzi hao wakware walikuwa wakifanya mapenzi wakiegemea dirisha ambapo mwanamke alidondoka na kuangukia kifudifudi huku mpenzi wake akimfuatia kwa juu.

Wapenzi hao walivunjika baadhi ya mifupa ya miili yao na walipata majeraha kichwani.

Lakini katika hali ya kushangaza, pamoja na kwamba walikutwa pembeni ya barabara wakiwa uchi, mwanamke alisisitiza kuwa hawakuwa wakifanya mapenzi bali wakifanyiana masihara.

Na katika kuleta utamu zaidi wa tukio hilo, mwanamke huyo na mpenzi wake waliwahishwa hospitali ambako huko walikutana na mume wa mwanamke ambaye naye siku hiyo hiyo aliwahishwa hospitali baada ya kudondoka toka kwenye paa la nyumba yake wakati akilifanyia marekebisho.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment