Aacha Ualimu na kuwa Msanii wa Ngono

Thursday, August 05, 2010 / Posted by ishak /


Mwalimu mmoja nchini Uingereza ameacha kazi yake ya ualimu wa sekondari na kuamua kuanza kazi mpya ya usanii wa filamu za ngono huku akitumiwa salamu za kutakiwa mafanikio na wanafunzi wake walioziona filamu zake kwenye internet.
Liselle Bailey mwenye umri wa miaka 30 aliacha kazi yake ya ualimu wa sekondari na kuanza kazi mpya kucheza na kuongoza filamu za ngono.

Wanafunzi wa mwalimu huyo waliobahatika kuona filamu zake kwenye internet walipigwa na butwaa lakini hawakusita kumtumia salamu za kumtakia mafanikio kwenye kazi yake hiyo mpya.

Mmoja wa wanafunzi wake aliyeitwa Daniel aliandika "Mwalimu Bailey tunakupenda, nakutakia mafanikio kwenye kazi yako mpya".

Mwanafunzi mwingine aliandika maoni kwenye internet "Mwalimu bora wa kiingereza, umepata kazi bora kuliko zote, hongera".

Mwalimu Bailey alikuwa akifundisha somo la kiingereza na somo la maigizo kwenye shule ya seminari ya Grindon Hall.

"Huu ulikuwa ni uamuzi wangu wa busara", alisema Bailey na kuongeza kuwa katika mwaka mmoja wa fani yake hiyo mpya ameweza kuwa nyota wa kampuni ya Joybear Pictures.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment