Atakayemuonyesha Obama Matiti Yake Kulipwa Dola Milioni 1

Wednesday, August 18, 2010 / Posted by ishak /


Bilionea mmoja wa nchini Marekani ameahidi kutoa zawadi ya dola milioni moja kwa mwanamke yoyote atakayejitokeza mbele ya rais wa Marekani, Barack Obama na kisha kumuonyesha matiti yake.
Bilionea Alki David ili kuitangaza tovuti yake ya "Battlecam" ameahidi donge nono la dola milioni 1 kwa mwanamke yoyote atakayekuwa wa kwanza kujitokeza mbele ya rais Obama na kisha kumuonyesha matiti yake huku akiwa amebandika lebo ya "Battlecam" kwenye kifua chake.

Sharti ya kushinda donge hilo nono ni kwamba tukio hilo lazima lionyeshwe LIVE kwenye tovuti ya Battlecam inayomilikiwa na bilionea huyo.

Awali bilionea huyo aliahidi kutoa zawadi ya dola laki moja lakini ameamua kuiongeza zawadi hiyo iwe dola milioni 1 baada ya watu kuona dola laki moja si donge nono.

"Watu wengi wanafikiria dola 100,000 hazitoshi kumfanya mtu azionyeshe sehemu zake nyeti kwenye hadhara, lakini dola milioni 1 ni pesa za kutosha kabisa", alisema bilionea Alki.

Alki alisema kwamba hadi sasa jumla ya watu 150 wameishajiandikisha kuwania zawadi hiyo.

Bilionea huyo alidai kuwa ameamua kumchagua Obama kwakuwa Obama ndiye kiongozi mkubwa wa dunia.

Bilionea Alki alizaliwa Lagos, Nigeria lakini anaishi Los Angeles, Marekani.

Ana nyumba tatu za kifahari nchini Uingereza na alitajwa kushika nafasi ya 45 katika listi ya matajiri waliopo Uingereza kwa mujibu wa gazeti la The Times la Uingereza.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment