Auza Bikira Yake Kwa Tsh. Milioni 500

Monday, August 09, 2010 / Posted by ishak /


Msichana mmoja wa nchini Hungary ambaye aliinadi bikira yake kwenye mtandao ili apate pesa za kuisaidia familia yake, amepata mteja ambaye ameinunua bikira yake sawa na Tsh. Milioni 500.
Msichana huyo mwenye umri wa miaka 19 anayejiita "Miss Spring" ameamua kuiuza bikira yake kwa mwanaume raia wa Uingereza ambaye atatoa paundi 200,000.

Msichana huyo alisema kuwa aliamua kuiuza bikira yake ili aweze kulipia gharama za masomo yake na pia aweze kulipa madeni ya mama yake.

"Familia yangu ina madeni na hatuwezi kuyalipa, mama yangu alikopa pesa ambazo alishindwa kuzilipa na kupelekea tupoteze nyumba yetu, nataka nilipe madeni yote", alisema msichana huyo.

"Pesa nilizopata sio nyingi sana kwani nitapoteza nusu yake kwenye kodi", aliongeza msichana huyo.

Msichana huyo alisema kuwa anajiandaa kwenda Uingereza ili aweze kumtunuku bikira yake mdau aliyetoa dau kubwa kuliko wote.

Mnada wa bikira ya msichana huyo ulianzia kwenye mtandao wa Ebay lakini ulimalizikia kwa njia ya email baada ya Ebay kuufutilia mbali mnada huo baada ya kugundua unahusisha uuzaji wa mapenzi.

"Nilikuwa nikiwasiliana na washindi wawili, mmoja raia wa Uingereza na mwingine raia wa Ireland, nimemchagua mwanaume wa Uingereza".

"Wote wanataka kunioa na kuitunza familia yangu lakini kwa sasa sifikirii kuishi maisha ya ndoa", alisema msichana huyo.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment