Mapenzi Yanapozidi....

Tuesday, August 31, 2010 / Posted by ishak /


Mfanyabiashara mmoja wa nchini Italia ambaye hakuweza kustahimili kupigwa kibuti na mpenzi wake, ametumia kiasi cha pesa sawa na Tsh. Milioni 30 kutengeneza toy ambalo linafanana kila kitu na mpenzi wake.
Mfanyabiashara huyo mwenye umri wa miaka 50, hakuweza kuvumilia kukimbiwa na mpenzi wake kiasi cha kuamua kutafuta mpenzi mpya wa bandia ambaye atakuwa naye maisha yake yote.

Mfanyabiashara huyo alitumia kiasi cha dola za kimarekani 18,000 kutengeneza doli la ngono (sex doll) ambalo lilifanana na mpenzi wake wa zamani kuanzia sura, macho mpaka kucha.

Mfanyabiashara huyo alichukua picha kadhaa za mpenzi wake huyo wa zamani na kumwambia mtengeneza madoli wa nchini Italia Diego Bortolin kuwa anataka atengenezewe doli ambalo litafanana na mpenzi wake isipokuwa liwe na matiti makubwa zaidi.

Bortolin alikataa kutaja jina la mfanyabiashara huyo lakini alisema kuwa hutengeneza madoli ya ngono ambayo hukaribia uhalisia ambayo huuzwa kwenye duka lake linaloitwa "Tentazioni" lililopo kwenye mji wa Treviso nchini humo.

"Alitaka mpenzi wake mpya awe na matiti makubwa na makalio makubwa", alisema Bortolin.

Kwa kawaida Bortolin huuza madoli anayoyatengeneza kwa dola 5,000 lakini dili hili la mfanyabiashara liligharimu pesa nyingi kwakuwa lilitakiwa lifanane kila kitu na mpenzi wake kuanzia sura, mpangilio wa meno mpaka kucha.

"Watu wataona kama amefanya kitu cha kipuuzi lakini mimi naona amepata mpenzi mpya mrembo wa maisha", alisema Bortolin.

Doli hilo lina uzito wa kilo 58 na urefu wa mita 1.6. "Ataweza kulikunja na kuliweka katika staili yoyote ile aitakayo", alimalizia kusema Bortolin.


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment