Mtoto Mnene Kuliko Wote Duniani

Friday, August 20, 2010 / Posted by ishak /


Ana umri wa miezi 10 lakini mtoto huyu wa nchini China ana uzito zaidi ya mtoto wa miaka sita.
Mtoto wa miezi 10 wa nchini China anayeitwa Lei Lei huenda akawa ndio mtoto mnene kuliko watoto wote duniani.

Lei Lei pamoja na umri wake huo mdogo ana uzito wa kilo 20 ambao kawaida ni uzito wa mtoto kuanzia umri wa miaka sita.

Lei Lei alizaliwa akiwa na uzito wa kawaida kama watoto wengine.

Lakini mbali ya maziwa ya mama yake, Lei Lei alikuwa akibugia kila kitu kilichokuwa mbele yake,

Lei Lei ambaye anaishi na wazazi wake kwenye jimbo la Hunan, amebatizwa jina la "Mtoto wa Michelin" na majirani zake.

Lei Lei amelazwa kwenye hospitali moja mjini humo akifanyiwa uchunguzi na madaktari ili kujua sababu ya unene wake.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment