Nyota wa Muziki Aliyewaambukiza Watu Ukimwi Anusurika Kwenda Jela

Friday, August 27, 2010 / Posted by ishak /


Nyota wa muziki wa Pop wa Ujerumani ambaye huku akijua kuwa ameathirika, alifanya mapenzi na wanaume bila kutumia kinga na kupelekea kumuambukiza ukimwi mpenzi wake mmoja, amenusurika kwenda jela baada ya kuhukumiwa kifungo cha nje cha miaka miwili
Mahakama ya mji wa Darmstadt nchini Ujerumani, imemhukumu kifungo cha nje cha miaka miwili, mwanamke nyota wa muziki wa pop wa nchini humo Nadja Benaissa kwa kosa la kumuambukiza ukimwi mpenzi wake.

Benaissa ambaye ni mmoja wa waimbaji wa kundi la muziki wa Pop la "No Angels", alipewa hukumu hiyo baada ya kupatikana na hatia ya kosa moja la kudhuru mwili.

Mwimbaji huyo maarufu wa nchini Ujerumani alikiri kufanya mapenzi na wanaume bila kutumia kinga bila ya kuwajulisha kuwa yeye ni muathirika.

Benaissa ambaye ni mjerumani mwenye asili ya Morocco, aliomba radhi mahakamani kwa kitendo chake hicho kwa kusema "Naomba radhi kwa moyo wangu wote, ningependa kuurudisha muda nyuma ili kuepuka vitendo nilivyofanya lakini siwezi kufanya hivyo".

Benaissa anadaiwa kufanya mapenzi na wanaume watatu kati ya mwaka 2000 na 2004 bila ya kuwataarifu kuwa yeye ni muathirika.

Benaissa alikuwa akijitambua fika kuwa yeye ni muathirika tangia mwaka 1999, nyaraka za mahakama zilisema.

Benaissa aligundulika ana ukimwi wakati wa ujauzito wake wakati alipokuwa na umri wa miaka 16.

Mmoja wa wanaume hao watatu ambaye ameishathibitishwa kuwa ameambukizwa virusi vya HIV vinavyosababisha ukimwi ndiye aliyemfikisha mahakamani Benaissa.

Kosa lililokuwa likimkabili Benaissa lingeweza kupelekea ahukumiwe kwenda jela miaka 10, lakini waendesha mashtaka walitaka ahukumiwe kifungo cha nje kwakuwa alikiri kosa lake na kuomba msamaha.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment