Nyota wa Uingereza Amhonga Kahaba Paundi 800 Kwa Usiku Mmoja

Monday, August 09, 2010 / Posted by ishak /


Nyota wa Uingereza na timu ya Tottenham Hotspurs, Peter Crouch ameingia kwenye skendo kubwa sana baada ya kumsaliti mchumba wake na kumhonga kahaba paundi 800(Takribani Tsh. Milioni 1.8) kwa usiku mmoja.
Peter Crouch alikuwa kwenye vakesheni nchini Hispania pamoja na mchumba wake mwanamitindo, Abbey Clancy.

Siku mbili baada ya kumaliza vakesheni yake, Crouch alishindwa kujizuia kumsaliti mchumba wake kwa kununua penzi toka kwa kahaba mwenye umri wa miaka 19, anayejiita Monica Mint.

Crouch alimhonga kahaba huyo, paundi 800 ili afanye naye mapenzi mara mbili ndani ya usiku mmoja, mara moja kwenye taksi na baadae hotelini kwake.

Akitoboa siri ya tukio hilo, Monica aliliambia gazeti la News of the World la Uingereza kuwa Crouch hakujivunga hata kidogo kununua penzi lake kwa kiasi kikubwa cha pesa.

"Hakuhofia watu kutuona nyuma ya taksi, alisisitiza tufanye mapenzi ndani ya taksi wakati tukielekea hotelini", alisema Monica.

"Nilikuwa sijui kuwa ana mchumba, bado siamini amenunua penzi langu wakati ana mwanamke mrembo amemuacha nyumbani kwake", alimalizia kusema Monica.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment